Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, January 30, 2013

TALAKA (2)

KUACHANA/TALAKA TALAKA ni amri inayotolewa na mahakama kuwaamuru wanandoa kuachana milele.Mume au mke anaweza kuiomba mahakama itoe talaka MATOKEO YA KUACHANA/TALAKA (i)Ndoa kuvunjika (ii)Mgawanyo wa mali zilizochumwa kwa pamoja na wanandoa (iii)Matunzo na malezi ya watoto kama wapo MUHIMU Kwa kawaida hairuhusiwi kuvunja/kutenganisha au kuomba talaka mahakamani kabla ya muda wa miaka miwili kupita tangu wanandoa hao waoane,isipokuwa kwa ruhusa/hati ya mahakama tu.Hati hiyo ya mahakama itatolewa ikiwa imethibitika kuwa mwombaji ana hali ngumu isiyo ya kawaida,isiyoweza kuvumilika kwa muda huo wa miaka miwili ITAENDELEA KESHO

No comments:

Post a Comment