Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, January 27, 2015

AUAWA KWA SHOKA,ANYOFOLEWA ULIMI,MENO NA JICHO LA KUSHOTO

WATU watatu wamefariki dunia mkoani Mbeya katika matukio tofauti yakiwemo mawili ya mauaji ya kinyama.

Miongoni mwa matukio ya mauaji hayo ni pamoja na la mkazi wa kijiji cha Mkutano wilayani Momba,Hamis Simwawa(25) aliyekutwa shambani akiwa ameuawa kwa kukatwa shoka shingoni na kisha kunyofolewa viungo vya mwili ikiwemo ulimi,meno ya chini na jicho la kushoto.

Kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya Barakael Masaki mwili wa Hamis ulikutwa Januari 26 mwaka huu majira ya saa 2:00 asubuhi katika kijiji cha  Mkutano kilichopo katika kata ya Nzoka wilayani Momba.

Kaimu kamanda Masaki alisema kabla ya mauaji kijana huyo aliitwa kwenda kusaidia shughuli za shamba na alipofika shambani ndipo walimuua kwa kumkata na shoka shingoni kabla ya kumnyofoa ulimi,meno ya chini na jicho la kushoto na kupeleka viungo hivyo kusikojulikana.

Alisema tukio hilo linahusishwa na imani za kishirikina na kufuatia mauaji hayo watu wawili wanashikiliwa aliowataja kuwa ni Kawawa Sinkala(31) na Emmanuel Sinkala(15) wote wakazi wa kijiji cha Mkutano.

Katika tukio la pili Kaimu kamanda Masaki alisema Mwinzala Sekele mwenye umri wa kati ya miaka 40 na 45 mkazi wa kitongoji cha Chang’ombe kilichopo kijijini Mshewe wilayani Mbeya aliuawa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za mwili wake na kundi la wananchi walioamu kujichukulia sheria mkononi.

Alisema mwili wa marehemu ulikutwa saa Januari 26 mwaka huu majira ya saa 5:00 asubuhi ukiwa umetelekezwa kijijini mshewe kata ya Bonde la Usongwe wilayani Mbeya.

Kwa mujibu wa kaimu kamanda Masaki inadaiwa kuwa chanzo cha mauaji hayo ni kulipiza kisasi kufuatia marehemu kutuhumiwa kuhusika na mauaji yaliyotokea awali Januari 24 mwaka huu majira ya saa tisa alasiri ambapo mkazi wa mkazi wa kijiji cha Mshewe Sekela Kaini alikutwa ameuawa na mwili wake kutupwa kwenye shamba la mahindi kijijini hapo.

Wakati huo huo mkazi wa Ilomba jijini Mbeya Joshua Mwaisanila(35) alifariki dunia baada ya kugongwa na lori lenye namba T 189 BLKs Semi Trailler lililokuwa na tela lenye namba  T 193 BLK lililokuwa likiendeshwa na Ahazi Cheyo(24) mkazi wa Iyunga jijini Mbeya.

Kaimu kamanda Masaki alisema ajali hiyo ilitokea Januari 26 mwaka huu saa tatu asubuhi maeneo ya Forest barabara kuu ya Mbeya/Tunduma na dereva wa lori hilo anashikiliwa na polisi wakati chanzo cha ajali kinachunguzwa.

No comments:

Post a Comment