Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, January 19, 2015

CBE YAKABIDHI MSAADA HOSPITALI YA WAZAZI META


                             HABARI KAMILI

MSAADA wa shuka wenye thamani  ya takribani shilingi milioni tano umetolewa na Chuo cha Biashara(CBE) kwa hospitali ya Rufaa Mbeya kitengo cha wazazi na watoto cha Meta.

CBE imetoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho yake ya kutimiza jumilei ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa chuo hicho nchini ikiwa ni wakati pia ambapo inajivunia mafanikio yake yakiwemo kusambaza matawi yake mikoani likiwemo la Mbeya.

Akikabidhi msaada huo leo,mkuu wa chuo cha CBE Prof Emmanuel Mjema amesema chuo kinathamini huduma za afya hudusani kitengo cha uzazi kutokana na kuwa kati ya maeneo muhimu yanayowezesha afya ya binadamu kuimarika.

Amesema kutolewa kwa shuka hizo kunadhihirisha wazi kuwa CBE inakijali kizazazi kilichopo na kijacho hivyo kuna kila sababu ya kuweka mazingira bora kwa mtoto anayezaliwa ili akue akiwa na afya bora na hatimaye maishani mwake kuja kuwa mtaalamu wa biashara akiwa miongoni mwa wadau wa chuo hicho.


Kwa upande wake Mkuu wa hospitali ya wazazi Meta Dk.John Francis amesema msaada huo umekuja kwa wakati muafaka kwani licha ya hospitali ya rufaa katika kitengo hicho kutokuwa na uhaba mkubwa wa vitendea kazi,bado vifaa vilivyopo havitoshelezi mahitaji.

Dk.Francis amesema kumekuwepo na ongezeko kubwa la akina mama na watoto wanaofika hospitalini hapo kuhitaji huduma za afya hivyo wadau wanapaswa kuendelea kutoa michango yao ya hali na mali ili huduma bora inayotolewa izidi kuwa endelevu.

No comments:

Post a Comment