Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, January 2, 2015

KIKUNDI CHA SAVE ORPHANS CHATOA MSAADA WA MWAKA MPYA KWA YATIMA

 Vitu mbalimbali vilivyokabidhiwa kwa kituo hicho

 Mwenyekiti wa kikundi cha Save Orphans Redson Kaisi akizungumza jambo kabla ya kukabidhi msaada
 Mkuu wa kituo Malezi ya Huruma Anna Kasile akibainisha namna watoto waishio kituoni hapo wanavyopokelewa na kulelewa.




                             HABARI KAMILI
KIKUNDI cha Save Orphans cha jijini Mbeya kimetoa msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Malezi ya Huruma kilichopo Simike jijini hapo.

Baadhi ya vitu vilivyokabidhiwa ni mchele,sukari,nyama,mafuta ya kupikia na ya kupakaa,sabuni za unga na za mche,madaftari na kalamu za wino na risasi.

Mwenyekiti wa kikundi cha Save Orphans Redson Kaisi amesema lengo la kutoa msaada huo ni kuwawezesha watoto kituoni hapo kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya kwa furaha kama ilivyo kwa watoto wengine.

Kaisi alisema kikundi hicho chenye wanachama wanne kimekuwa kikitoa misada kwa vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima kutokana na kutambua mahitaji ya watoto hao ambao baadhi ya wanajamii wamekuwa wakiwatenga.

Ameitaka jamii kwa namna inavyoguswa kujitolea kuwasaidia watoto yatima ili kuwawezesha kuishi maisha mazuri na kutimiza ndoto zao kwa kuwajengea mazingira bora ya kuishi.

“Asilimia kubwa ya jamii tumekuwa tukijisahau kwa kuwapa huduma za msingi watoto tunaoishi nao majumbani pekee.Tunasahau kuwa wapo ambao hawana wazazi wala walezi ambao nao wana uhitaji kama wale tunaoishi nao.Tukiendelea kuwasahau tujue tunajenga tabaka la kiubaguzi ndani ya jamii zetu” alisema Kaisi.

Akipokea msaada huyo,mkuu wa kituo Malezi ya Huruma Anna Kasile amesema amekuwa akiwalea watoto kituoni hapo katika mazingira magumu kutokana na kutokuwa na chanzo cha mapato zaidi ya misaada ya wadau mbalimbali.

Kasile pia amelalamikia uwepo wa watu ambao wamekuwa wakimbeza kwa kumuita mtu aliyepungukiwa na akili na ndiyo sababu anaendelea kupokea na kuishi na watoto waio wake.

Hata hivyo amesema changamoto hizo haziwezi kumkatisha tama,badala yake anazichukulia kama chanhu ya kuongeza upendo wake kwa jamii ya watoto yatima na kuomba wadau zaidi kuendelea kushirikiana naye katika kutimiza malengo na ndoto za watoto kituoni hapo.

No comments:

Post a Comment