Na Joachim Nyambo.
“SIWEZI kuisahau siku ya Julai 7
mwaka 2011 maishani mwangu.Maana ni siku yenye historia kubwa kwangu.Ni siku niliyojikuta
siwezi tena kutunza heshima ya ndoa kwa wake zangu” yalikuwa maneno yake Mwiguru Nguro alipozungumza
nami mnamo Machi 2012.Ni siku nyingine tena nilipokitembelea kijiji cha Kapunga
wilayani Chunya na kuzungumza na mkazi huyu.
Mwigulu ambaye kwa wakati huo
alikuwa na umri wa miaka 45 alikuwa ni muwe wa wake wawili.Kati ya wake hao mke
mkubwa alikuwa amebahatika kuzaa watoto watatu na mke mdogo mtoto mmoja.Yeye
pamoja na wake zake na watoto hao walikuwa wakishi katika kitongoji cha Mkanada
kijijini Kapunga.
Kijiji wanachoishi ni kile ambacho
wakazi wake walikuwa na mgogoro wa muda mrefu na kampuni ya Expot Trading
kuhusiana na mpaka kama nilivyokusimulia kwenye toleo la kwanza la makala haya.Wakazi
wa kijiji hicho walikuwa wakidai kijiji chao kipo kihalali lakini mwekezaji akipinga
na kusema kijiji kiko ndani ya shamba lake.
Mvutano huo wa kimipaka ndiyo ulikuwa
chanzo cha matukio mengi na malalamiko mbalimbali kwa pande zote.Tukio la Mwigulu
ni miongoni mwa yale ya kinyama yaliyoelezwa na kijiji kuwa yamefanywa na
mwekezaji kwa wakati huo.
Mwigulu ambaye ni mfugaji wa kabila
la Kisukuma alisema tarehe hiyo asiyoweza kuisahau alikuwa na mwenzake
waliyekuwa wakiendelea kulisha mifugo yao kama kawaida yao.Anasema siku hiyo
walikuwa wakichunga ng’ombe wao karibu na shamba la mwekezaji.
Alisema wakati wanaendelea na
shughuli hiyo ghafla mmoja wa watumishi wa kampuni ndogo ya Kapunga Rice
Project iliyo chini ya Expot Trading Company aliyemtaja kwa jina moja la Gerry
akiwa na walinzi walifika na gari ya kampuni na kuanza kuwafanyia vurugu.Lengo
lao lilikuwa kuwakamata ng’ombe wao wakidai wameingizwa katika eneo la
mwekezaji.
“Walijaribu kuwaswaga ng’ombe ili
wawapeleke kambini kwao lakini sisi nasi tukawa tunawaaswaga wasiende
huko.Baada ya mifugo yetu kuona inalaazimishwa na wasu isiyo na mazoea nayo
baadhi ilianza kucharuka na ndipo mlinzi aliyekuwa na bunduki akapiga risasi na
kumuua ng’ombe mmoja papo hapo na mwingine kumjeruhi”
“Hiyo haikutosha.Tukiwa tunaendelea
kuikusanya mifugo yetu.Gerry aliingia kwenye gari na baada ya kuiwasha akaanza
kunifuata nilipo kwa lengo la kunigonga.Nilijaribu kujitetea kwa kukimbia
nikiikwepa gari.Mara ya kwanza alinikosa,yapili nikafanikiwa pia kukwepa
laakini mara ya tatu sikuweza maana nilijikuta nimetumbukia kwenye kishimo
kidogo na ndipo gari yake ikanigonga kiunoni.Inaonekana kwenye ngao ya gari
yake kulikuwa na chuma kilichonichoma vibaya sehemu ya haja kubwa”
“Nilipata maumivu makali mno kiasi
nikapoteza fahamu.Wasamariaa wema walinibeba na kunipeleka katika hospitali ya
Chimala.Nilikaa hapo lakini baadaye ikaonekana huduma ninayopaswa kupewa
haiwezi kupatikana hapo maana nilikuwa nimeumia vibaya”
Alisema kutokana kuhitaji huduma
katika hospitali iliyo na uwezo zaidi ya hiyo ilimlazimu kwenda katika
hospitali teule ya Ifisi iliyopo Mbeya vijijini.Aliendelea na matibabu tangu
Julai 18 hadi Septemba 7 mwaka 2011.
Akiwa hospitalini hapo aliambiwa na
madaktari kuwa mfumo wake wa uzazi ulikuwa umehaaribiwa hasa baada ya kuoza
kwakuwa alichelewa kufanyiwa oparesheni.Alipaswa kufanyiwa oparesheni hiyo muda
mfupi tu baada ya kugongwa lakini kutokana na kuchelewa baadhi ya mishipa
ilikwisha anza kuoza.
“Niliambiwa kuwa baada tu ya
kufikishwa katika hospitali ya Chimala nilipaswa kufanyiwa oparesheni hiyo na
kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kupona na hatimaaye kuwa na uwezo wa
kusimamisha uume kama awali.Ina maana kule walipaswa kunisafisha na kisha
kushona jeraha langu.Kutokana na kuchelewa kufanyiwa lilivunda na kuozesha
baadhi ya mishipa hivyo nikaambiwa huenda nikapona lakini inaweza kuchukuaa
muda mrefu kidogo”
“Katika kipindi hicho chote mhusika
hakuwahi kunitembelea hata siku moja wala kuchangia gharama za matibabu
yangu.Mpaka hivi sasa nazungumza na wewe hakuna chochote ninachoweza
kufanya.Si kazi wala tendo la ndoa maana kiuno change hakijapona natembea kwa
msaada wa magongo na pia uume wangu hauwezi kusimama kama awali”.
Hata hivyo Mwiguru alinambia
hajakata tamaa.Bado alikuwa na imani kuwa huenda akapona na siku moja
akaendelea kutunza heshima katika ndoa zake.Aliwashukuru wake zake wote kwa
kuendelea kumheshimu licha ya yeye kukosa uwezo wa kuwaridhisha kwa kuwapa haki
yao ya msingi ya tendo la ndoa kwa wakati huo.
“Pamoja na matatizo yangu
wameendelea kuwa na uvumilivu naamini ni kwakuwa wao pia wana subira wakiamini
ipo siku nitapona naa kurejea katika hali yangu ya kawaida.Hakuna yeyote kati
yao aliyenidharaau kwa kuisaliti ndoa yetu”
“Si kwamba wanakijiji wanamjengea majungu
mwekezaji bali vitendo anavyowafanyia haviwapendezi maana ni vya
kinyama.Chukulia mfano kama sisi tulikuwa na makosa kwa nini asifuate njia
zinazostahili.Vyombo vya sheria vipo ambavyo vingetuita na kutuwajibisha.Kwa
nini ajichukulie sheria mikononi na kunipa ulemavu kama huu.Kwa nini aue mifugo
yetu”.Anasema
“Kama mimi migogoro ya mashamba alio
nayo na wanakijiji wenzangu wala hainigusi sana maana haihusishi eneo la makazi
yangu wala mashamba yangu sasa kwa nini nianze kumjengea visa.Tatizo ni haya
anayotufanyia.Kutufanyia unyama wa namna hii na pia kuuwa na kujeruhi mifugo
yetu”
“Sasa tunajiuliza hivi serikali
ilimleta mwekezaji itusaidie wananchi au ndiyo ilimleta atuangamize.Maana
anachokifanya si kutusaidia wanaKapunga bali kutuangamizaa.Si mimi tu amewahi
kung’oa madaraja yanayotumiwa na wakazi wa kijiji hiki kuvuka kwenda eneo la
Mpunga mmoja kuliko na mashamba yao.Alifanya shughuli hiyo usiku na mvua kubwa
zikanyesha matokeo yake watu wameamka wanakwenda kuvuka wakijua daraja lipo
wakasombwa na maji.Wapo waliopoteza maisha kwa kufa maji siku hiyo ”
Haya yalikuwa mateso mengine makubwa
yaliyowakumba wakazi wa kijiji cha Kapunga kutokana na ardhi yao waliyoamua
kumkabidhi Mwalimu Nyerere kwa maendeleo ya taifa lao.Hay pia yaliendelea kuzua
hisia kwa wakazi hawa kutamani Baba wa taifa hili afufuke ili arejeshe ardhi
yao kwakuwa sasa ilikuwa imegeuka Jehanamu kwao.
.................... ITAENDELEA KESHO...................
No comments:
Post a Comment