Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, February 29, 2016

MOTO WATEKETEZA BWENI LA WANAFUNZI IYUNGA SEC




WANAFUNZI 95 katika shule ya sekondari ya wavulana ya Iyunga jijini Mbeya hawana mahali pa kulala kufuatia moto mkubwa kuteketeza Bweni lao leo (Feb 29) lililokuwa likifahamika kwa jina la Mkwawa.

Kwa mujibu wa mkuu wa shule hiyo Edward Mwantimwa moto huo umezuka majira ya saa 4:00 asubuhi wakati wanafunzi  wakiwa darasani wakiendelea na masomo na baadaye Askati wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji walifika na kufanikiwa kuuzima ukiwa umeteketeza bweni lote.

Mwantimwa amesema pamoja na kutokuwepo kwa mwanafunzi aliyejeruhiwa moto huo umeteketeza vifaa mbalimbali vikiwemo vitanda,magodoro na nguo za wanafunzi 95 waliokuwa wakilitumia bweni hilo huku bweni jirani la Nyerere likiadhiriwa kidogo pia.

Akizungumzia chanzo cha tukio hilo,mkuu huyo wa shule moto amesema umetokana na hitilafu ya umeme kwenye soketi ambayo ipo karibu na mlangoni lakini hakubainisha iwapo soketi hiyo ilikuwa ikitumika wakati tukio likitokea.

Amesema kutokana na moto kuanzia katika eneo la mlango ilikuwqa vigumu kwa waokoaji kuweza kuingia ndani na kuokoa vitu vilivyokuwemo.

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Mbeya Nyirembe Munasa amesema  sababu ya moto huo ni uchakavu wa miondombinu ya shule hiyo kongwe iliyojengwa tangu wakati wa utawala wa Mkoloni.

Munasa amesema kutokana na uchakavu wa majengo wanafunzi pamoja na watumishi shuleni hapo wanapaswa kuchukua taadhari katika utumiaji wa miundombinu hiyo hasa ya umeme, vyoo, na maji ambayo inaokena inauchakavu mkubwa.

Mkuu huyo wa wilaya amemtaka kaimu mkurugenzi wa halmaashauri ya jiji la Mbeya Dk Samwel Lazaro kununua vifaa  muhimu kwa mahitaji wa wanafunzi wakati mpango wa kukarabati jengo la bweni lililoungua ukiendelea kufanyiwa kazi.Thamani halisi ya hasara iliyopatikana bado haijafahamika.

No comments:

Post a Comment