Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, February 4, 2016

MASHABIKI MBEYA CITY WAKATA TAMAA

MWENENDO mbaya wa timu ya Mbeya City katika ligi kuu Tanzania bara umeonekana kuwachanganya wadau wa soka mkoani hapa kiasi cha kuanza kuutupia lawama uongozi wa timu hiyo sambamba na Chama Cha Soka mkoa wa Mbeya(MREFA).

Katika maeneo na nyakati tofauti wadau hao wameelezea masikitiko waliyonayo juu ya mweneno wa Mbeya City  huku wakisisitiza jitihada za haraka kufanyika ili kuinusuru timu hiyo kushuka daraja.

Baadhi ya wadau wanasema matokeo mabovu kwa michezo ya timu hiyo inatokana na usajiri mbovu,wengine kushuka kwa nidhamu ya wachezaji ni chanzo huku wengine nao wakisema kutokuwepo kwa maelewano baina ya uongozi wa timu na Mrefa ni tatizo.

“Tunashangaa timu inafanya vibaya viongozi wako kimya hatuoni hamasa yoyote iliyo shirikishi ili kutafuta ufumbuzi.” Alisema mmoja wa wadau hao Godfray Davis

Naye Mwalimu Josephat Antony amesema jitihada za dhati za haraka zinapaswa kufanyika ili kuinusuru Mbeya City akisema kuipandisha timu inaposhuka daraja ni kazi kubwa hivyo ni muhimu kutoruhusu hali hiyo kutokea.

Kwa upande wake Edward Mwambusye amesema kusajiri wachezaji wakongwe ndiyo kunakoiponza Mbeya City kwakuwa wachezaji hao wanajioni fahari na hivyo hawaoni sababu ya kujituma wawapo uwanjani.

Anasema kinachotakiwa kwa sasa ni wadau kuona uwezekano wa kuikoa timu hiyo isishuke daraja lakini matokeo yanayopatikana yawe fundisho kwa timu hiyo katika msimu mwingine wa usajiri.

Akizungumzia suala la ushirikiano baina ya Mrefa na uongozi wa Mbeya City,katibu wachama hicho cha soka mkoa wa Mbeya Seleman Haroub amesema si kweli kuwa pande hizo haziwasiliani na badala yake akasema ipo mikakati mbalimbali inayofanyika ili timu hiyo isishuke daraja.

Haroub amesema aliwahakikishi wadau wa soka ndani na nje ya mkoa wa Mbeya kuwa Mbeya City haitashuka daraja na mkakati uliopo hivi sasa ni kuhakikisha kila mchezo inaocheza inaibuka na pointi tatu zote.

No comments:

Post a Comment