Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, February 11, 2013

MREFA YATANGAZA WAJUMBE WA KAMATI ZAKE

CHAMA cha soka mkoani Mbeya(MREFA) kimeteua wajumbe wa kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya Habari,Uenezi na Mawasiliano inayohusisha pia waandishi wa habari akiwamo mkurugenzi mtendaji wa Blogu ya Lyamba Lya Mfipa.
Mwenyekiti wa MREFA Elias Mwanjala alitaja wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni Lwitiko Mwamundela atakayekuwa mwenyekiti,Blandy Nelson ambaye ni katibu na wajumbe ni Joachim Nyambo,Charles Mwakipesile na Saleh Kupaza, Kwa upande wa kamati ya Uchumi Fedha na Mipango mwenyekiti ameteuliwa Omary Mahinya,Emanuel Kavenga ni katibu na wajumbe ni Teddy Karua,Fidelis Mwampoma,Agustino Sanga,Ayasi Njalambaha na Ambakisye Minga. Kamati ya Ufundi,Vijana na Maendeleo ya wanawake mwenyekiti ni Willium Mwamlima,katibu ni Elizabeth Kalinga na wajumbe ni Juma Mwambusi,Alex Lusekelo na Lucas Kasmiri wakati kamati ya waamuzi mwenyekiti ni Sadiki Jumbe,katibu ni John Kanyenye,wajumbe ni Paul Mwanjabike,Mwanahamis Muya na Albert Mwakasege. Kamati ya Mashindano Juma Kila ni mwenyekiti,katibu ni Dickson Sinkwembe,wajumbe ni Joel Kasebele na Omary Upuu,kamati ya Uchaguzi mwenyekiti Basilius Namkambe anaendelea na nafasi yake na wajumbe ni Shaaban Robert,Bakari Mketo na Daud Malimali. Mwanjala alisema balaza la wadhamini wajumbe wake ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapundizi(CCM) wilayani Kyela Dk.Hunter Mwakifuna,mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela,Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mbarali Adam Mgori,mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe tawi la Mbeya dk Ernest Kihanga na mfanyabiashara Thom Mwang’onda. “Kamati ya utendaji kwa kuzingatia majukumu iliyo nayo imeunda pia kamati ya masoko ambayo itakuwa na wajumbe Francis Mwasamwene,Gabriel Shawa na Claud Chawene kutoka kampuni ya bia ya TBL,David Bulegi na Priscar Kalinga kutoka kampuni ya Saruji ya Mbeya Cement na Uzia Mgala wa kampuni ya simu ya Vodacom”

No comments:

Post a Comment