Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, February 7, 2013

TALAKA (4)- JINSI YA KUPELEKA SHAURI LA KUVUNJA NDOA AU KUTENGANA MAHAKAMANI

Kabla shauri hilo halijapelekwa mahakamani,ni lazima lipitie kwenye balaza la usuluhishi la ndoa linalotambuliwa kisheria.Mwanandoa anayetaka kufanya hivyo anaweza kupeleka shauri hilo katika balaza la usuluhishi la ndoa ambalo linaweza kuwa la kidini au balaza la usuluhishi la ndoa la kata.Balaza linatakiwa kuwasikiliza au kuwasuluhisha wanandoa.Endapo balaza litashindwa kuwasuluhisha,litatoa taarifa/hati itakayowasilishwa mahakamani juu ya kushindwa huko ili mahakama iendelee kuamua itakavyoona inafaa.Hata hivyo sharti la kupeleka shauri la ndoa kwenye balaza la usuluhishi linaweza kuepukwa endapo tu itathibitika kuwa zipo sababu za msingi za kufanya hivyo.ITAENDELEA KESHO..........

No comments:

Post a Comment