Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, February 10, 2013

WATATU WATIMULIWA KAZI MBOZI

HALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya imewafukuza kazi watumishi wake watatu na kutoa onyo kwa wengine kadhaa kutokana na makosa mbalimbali ya ukiukwaji wa sheria za utumishi wa umma. Adhabu hiyo ilitolewa kwa watumishi hao baada ya kikao cha balaza la madiwani kulazimika kujigeuza na kuwa kamati kisha kujadili tuhuma mbalimbali zilizokuwa zinawakabili baadhi ya watumishi wengi wao wakiwa ni maofisa watendaji wa vijiji na kata. Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Elick Ambakisye aliwataja waliofukuzwa kazi kuwa ni pamoja na mkaguzi msaidizi Adela Shayo ambaye hajafika katika kituo chake cha kazi kwa zaidi ya miezi sita pasipo mwajiri wake kuwa na taarifa yoyote. Ambakisye aliwataja wengine kuwa ni ofisa mtendaji wa kijiji cha Kilimapimbi kata ya Isandula Joseph Mwashilindi na Abel Kandonga wa kijiji cha Senga ambao pamoja na makosa mengine pia walikuwa hawasomi mapato na matumizi ya vijiji vyao. Mwenyekiti huyo pia alisema halmashauri imeamuru kuwaandikia barua za onyo maofisa watendaji wengine 21 pamoja na barua za pongezi kwa maofisa watendaji wawili walioonekana kufanya shughuli zao kwa ufanisi mkubwa.

No comments:

Post a Comment