Tuesday, February 5, 2013
TALAKA (3)
MAMBO YA MUHIMU KUZINGATIWA KABLA YA KUTOA TALAKA......
Kwa kawaida mahakama hutoa talaka inapothibitika kwamba ndoa hiyo imevunjika kiasi cha kutokurekebishika tena kwa kuangalia mambo au vigezo vifuatavyo
(a)Ikiwa mmoja wa wanandoa hao atathibitika kufanya uzinzi(Ugoni)
(b)Ikiwa mmoja wa wanandoa hao alithibitika kumfanyia ukatili wa kimwili au kiakili mwanandoa mwenzake au watoto wao
(c)Iwapo itathibitika kuwa mmoja wa wanandoa hao amemtelekeza mwenzake na kwenda kuishi mbali au kumtelekeza akiwa ndani ya nyumba(Kwa kuhama chumba,kitanda au kuishi nyumba ya pili kati ya wanazomiliki bila ridhaa/idhini ya mwenza wake)
(d)Uasi au utoro
(e)Kutelekeza kwa makusudi
(f) kutengana kwa hiari au kwa amri ya mahakama kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu
(g)Kifungo kisichopungua miaka mitano au cha maisha
(h)Kichaa kisichotibika kilichothibitishwa na madaktari bingwa wa akili wasiopungua wawili
(i)Tofauti ya itikadi za kidini au siasa
ITAENDELEA KESHO.................
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment