Sunday, February 10, 2013
WAPELEKWA SEKONDARI KUJAZA VYUMBA
ASILIMIA 70 ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari mwaka huu wilayani Mbozi mkoani Mbeya hawana sifa za stahili za kujiunga na kidato cha kwanza.
Asilimia hiyo ni ya wanafunzi 2,276 walioteuliwa kuingia kidato cha kwanza katika shule za sekondari za wilayani hapa kati yao wakiwamo wasichana 1,143 na wavulana 1,133.
Mkuu wa wilaya ya Mbozi Dk.Michael Kadege aliyasema hayo katika kikao cha balaza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo na kuwataka madiwani na wadau wengine kuangalia ni namna gani wanaweza wakainusuru elimu wilayani kwao.
Dk.Kadege alisema Utafiti uliofanywa umebaini kuwa kati ya wanafunzi hao waliochaguliwa hawakupata alama za ufaulu za A,B na C badala yake ililazimu kuchukua kuanzia waliopata alama D hadi F ili kupata wanafunzi wa kujaza mvyumba katika shule za sekondari.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment