Monday, March 31, 2014
BABA AHUKUMIWA MIAKA 65 KWA KUMPA MIMBA MTOTO WAKE WA KUMZAA.
MAHAKAMA ya wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya jana(Machi 31) imemhukumu
kutumikia kifungo cha jumla ya miaka 65 jela mkazi wa mtaa wa Uhamila
katika mji mdogo wa Rujewa kutokana na makosa matatu tofauti
yaliyotokana na kumpa ujauzito mwanaye wa kumzaa.
Mshitakiwa aliyehukumiwa kifungo hicho ni Benjamin Muyinga(48) ambapo
mashitaka aliyokuwa akikabiliwa nayo mahakamani hapo ni Kufanya
mapenzi na mtoto wake,kubaka mtoto wake na la tatu ni kumpa mamba
mwanafunzi.
Awali ilielezwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa jeshi la
polisi Mazoya Luchagula,mbele ya hakimu mfawidhi Kinabo Minja kuwa
mnamo Oktoba 18 mwaka 2013 mwanafunzi(jina linahifadhiwa) aliyekuwa na
umri wa miaka 14 alikuwa mjamzito.
Luchagula alisema walimu wa shule hiyo ndiyo walitilia shaka suala la
mwanafunzi huyo aliyekuwa darasa la tano katika shule ya msingi Ibara
iliyopo Rujewa kuwa alikuwa na ujauzito na ndipo alipelekwa hospitali
na kwenda kukutwa akiwa na mamba ya miezi minne.
Alisema baada ya kuhojiwa mwanafunzi huyo alisema kuwa ujauuzito
ulikuwa wa baba yake mzazi waliyekuwa wakiishi naye wawili nyumbani
kwao kufuatia baba huyo kutengana na aliyekuwa mkewe ambaye hivi sasa
anaishi jijini Mbeya.
Alisema mwanafunzi huyo alibainisha namna alivyokuwa akiishi na baba
yake baada ya wazazi wake kutengana na ndipo baba yake akamgeuza
mwanaye huo kuwa mkewe ambapo alikuwa akilala naye na kufanya naye
mapenzi hadi ilipobainika kuwa na ujauzito huo.
Kutokana na kitendo kilichofanywa na mzazi huyo kutokubalika katika
jamii ya watanzania,mwendesha mashitaka aliiomba mahakama hiyo kutoa
adhabu kali kwa mshitakiwa ili kumpa fundisho yeye na wazazi wengine
wenye tamaa zenye kusababisha ukatili dhidi ya watoto wao.
Kufuatia kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo,hakimu
mfawidhi Minja alimhukumu mzazi huyo katili kutumikia kifungo cha
jumla ya miaka 65 jela kwa makosa hayo matatu kitakachotekelezwa kwa
wakati mmoja ili iwe fundisho kwa wazazi wenye tabia hizo.
Hakimu huyo alimhukumu mshitakiwa kutumikia jela miaka 30 kwa kosa la
kufanya mapenzi na mtoto wake,miaka 30 mingine kwa kubaka mtoto wake
na miaka mitano jela kwa kumpa mamba mwanafunzi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment