Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, May 12, 2014

MUST WAZINDUA MPANGO WA KUHAMASISHA WANAWAKE KUSOMA MASOMO YA UHANDISI,SAYANSI NA TEKNOLOJIA(WITED)

.Hizi ni baadhi ya kazi za kitaalamu zilizofanywa na wanafunzi wanawake katika chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya(MUST).Kazi hili zilioneshwa katika hafla ya uzinduzi wa mpango wa kuhamasisha wanawake kusoma masomo ya Uhandisi,Sayansi na Teknolojia Albertina Leonard Mwenyekiti WITTED na mkufunzi idara ya sayansi na biashara akisoma taarifa fupi ya mpango wa WITED Naibu Makamu wa chuo cha MUST idara ya Taaluma,Utafiti na ushauri Dk Noel Mbonde ambaye alisema bado chuo hicho kinakabiliwa na changamoto ya uhaba wa wanafunzi wa kike kutokana na jamii kujengeka katika fikra ya mafunzo ya ufundi ni ya wanaume. Alisema kwa sasa kati ya wanafunzi 3442 waliopo chuoni hapo wanafunzi wa kike ni 640 pekee aliosema kati yao 533 wanachukua stashahada huku wengine 107 wakiwa wanachukua shahada. Mkurugenzi msaidizi Wizara ya Sayansi na Tknolojia idara ya Sayansi na Ubunifu Dk.Magreth Komba aliwataka walimu wa masomo ya sayansi kuwa wabunifu wa mbinu mbadala za ufundishaji masomo hayo ili wanafunzi hususani wanawake wasiyakimbie

No comments:

Post a Comment