UCHAGUZI wa serikali za mitaa kwa mkoani Mbeya mpaka muda wa kupiga kura unamalizika hali imekuwa shwari na zoezi limekwenda kwa amani na utulivu.
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi ameiambia Lyamba Lya Mfipa kuwa mpaka muda
wa kumaliza zoezi la kupiga kura hakuna vurugu zozote zilizokuwa zimeripotiwa.
Kamanda Msangi amesema awali yalikuwepo mapungufu
madogo madogo katika baadhi ya vituo ikiwemo kukosewa kwa fomu ambapo baadhi
zilionekana kuwa na majina ya wagombea yasiyoendana na nembo za vyama vyao.
Amesema pia kuna baadhi ya vituo wasimamizi na
mawakala walichelewa kufika hivyo
kusababisha zoezi la upigaji kura kuchelewa kiasi lakini akasisitiza kuwa
kasoro zote zilitafutiwa ufumbuzi kwa haraka na zoezi likaendelea.
No comments:
Post a Comment