Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, December 4, 2014

NEEMA MWAKALINGA AZINDUA ALBAMU YA KILA JAMBO NA WAKATI

                              

  Neema akiwaongoza wasaidizi wake kutumbuiza kwenye hafla ya uzinduzi wa albamu yake.


 Mshereheshaji maarufu jijini Mbeya Beny Benjamini(Dauble B) akisherehesha katika hafla hiyo




        Sehemu ya vipande vilivyopo katika Video ya nyimbo zilizopo katika albamu iliyozinduliwa ikionesha Neema anavyoimba kwa hisia.


 Wadau waliojitokeza kumsindikiza Neema kwenye uzinduzi wakimiminika kumpongeza kwa kazi nzuri aliyoifanya






 Neema akijiandaa kukabidhi moja ya nakala za albamu yake kwa mgeni rasmi
 Mzee wa kanisa akizungumza neno kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua albamu.




                                         

                                            HABARI KAMILI

WASANII wakongwe wa nyimbo za Injili nchini wameaaswa kuwa na ushirikiano na wasanii wachanga ili kuwajengea msingi bora wa kudumu katika utoaji wa huduma hiyo.

Ombi hilo lilitolewa jana na msaanii anayechipukia katika muziki wa injili Neema Mwangalika wakati wa uzinduzi wa albamu yake ya kwenze aliyoipa jina la Kila Jambo na Wakati.

Katika uzinduzi wa albamu hiyo uliofanyika kwenye kanisa la Wapo Misheni International la Airpot jijini hapa Neema alisema wasanii wachanga wanahitaji kwa kiasi kikubwa ushirikiano wa wakongwe.

Alisema kwa kuwepo kwa ushirikiano wa pamoja kutawezesha sanaa ya muziki wa injili kuendelea kukua na kuwa na mvuto mkubwa zaidi.

“Ni kweli wakongwe wanakuwa na uzoefu mkubwa katika muziki huu.Lakini pia wasanii wanaochipukia nao wana mapya wanayoweza kuyaleta na kuwasaidia wakongwe.Hivyo kuna haja ya pande zote kushirikiana kwa pamoja”

“Sasa tukiendelea kujiweka katika makundi mawili tofauti.Wakongwe wakasema wabaki kama walivyo.Wachanga nao wakaachwa peke yao ni changamoto nyingine katika muziki wetu” alisema Neema.

Hata hivyo Neema alisema hakuna sababu ya wasanii wachanga kukatishwa tama na vikwazo wanavyowekewa na wakongwe badala yake wanapaswa kuendelea kujipa moyo huku wakiongeza ubunifu katika utendaji kazi wao.

Akizungumzia changamoto ya uandaaji wa muziki wa Injili,msanii huyo alisema ukosefu wa mtaji wenye kutosheleza mahitaji ni tatizo linalokwamisha wasanii wengi wanaochipukia.

Akizindua albamu ya Kila Jambo na Wakati,afisa mtendaji wa kata ya Iziwa jijini Mbeya Amanyisye Sageme pamoja na kuahidi kiasi cha shilingi 600,000 aliwataka wasanii wa nyimbo za injili kuzingatia maadili yanayozingatiwa na vitabu vitakatifu.

Aliwataka wasanii pia kuhakikisha wanadumisha amani na utulivu wan chi kupitia sanaa yao sambamba na kujitambua kama kioo cha jamii chenye kutumainiwa katika kutoa mafundisho ya maadili mema.

Albamu ya Kila Jambo na wakati ina nyimbo Pigana nao Bwana,Ninasifu Jina,Nataka niwe juu,Omba sana,Matendo yako,Mahali nimefika,Umeweka wimbo na Nioshwe na wewe.


No comments:

Post a Comment