Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, December 11, 2014

WASICHANA WAHIMIZWA KUKIMBILIA MASOMO YA UFUNDI NA SAYANSI

 Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari za jijini Mbeya wakifuatilia matukio kwenye Tamasha la kuhamasisha wanafunzi wa kike kujiunga na Masomo ya Ufundi na Sayansi lililofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere katika chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya(MUST)



 Naye mtafiti toka Taasisi ya Utafiri wa Kilimo katika kituo cha utafiki wa kilimo ya Mart Uyole Pia Urio akiwaasa wanafunzi wa kike kupenda masomo ya Sayansi
  Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari za jijini Mbeya waliohudhuria tamasha la kuhamasisha wanafunzi wa kike kujiunga na Mafunzo ya Ufundi na Sayansi katika chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya(MUST) wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa masuala ya sayansi

                                     HAHABARI KAMILI
WAZAZI kutowajengea mazingira mazuri ya kuwahamasisha watoto wao kuyapenda masomo ya Sayansi tangu wangali wadogo kumetajwa kuwa moja ya sababu zinazochangia watoto wa kike kutoyapenda masomo hayo.

Hayo yalibainishwa na wadau mbalimbali wa Masomo ya Sayansi kwenye tamasha ya kuhamasisha vijana kujiunga na M,afunzo ya Ufundi na Sayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya(MUST).

Miongoni mwa wadau waliozungumzia changamoto za Masomo ya Sayansi kwa wanafunzi wa kike ni walimu wa shule za sekondari ambao walisema jamii hususani wazazi wamekuwa wakichangia watoto kutoyapenda masomo hayo.

Mwalimu David Ngonyani kutoka shule ya sekondari ya Samora Machel ya jijini Mbeya alisema watoto wa kike wanayaogopa masomo ya Sayansi kutokana na uelewa mdogo waliojengewa kutoka kwenye familia zao kuwa ni magumu.

“Tangu mtoto anapokuwa nyumbani anajengewa uelewa kisaikolojia kuwa masomo ya Sayansi ni magumu na hawayawezi.Na pia familia hizi pia zinashiriki kuwapotosha watoto tangu wakiwa ni wadogo kuwa upatikanaji wa ajira kwa waliosoma sayansi ni mgumu ikilinganishwa na waliosoma sanaa” alisema mwalimu Ngonyani.

Naye Mwalimu Vaileth Msigwa wa sekondari ya Mwakibete alisema saikolojia ya kuyaogopa masomo ya sayansi inajengwa kwa wanafunzi tangu shule ya msingi hadi sekondari.

Kwa upande wake Mwalimu Helena Masalu kutoka shule ya sekondari ya Samora Macheri alisema wazazi wanapaswa kuwajibika kwa kuwavutia watito wao kuyapenda masomo ya sayansi tangu wangali wadogo kwa kuwaambia ukweli juu ya faida za kusoma masomo hayo.

Aawali Kaimu Makamu mkuu wa chuo cha Must Prof Emanuel Luoga alisema jittihada zinazofanywa na wadau mbalimbali wa masuala ya Sayansi ndani na nje ya nchi zimesaidia kuongezeka kwa udahili wa wanafunzi wa wa kike chuoni hapo.

Naye mtafiti toka Taasisi ya Utafiri wa Kilimo katika kituo cha utafiki wa kilimo ya Mart Uyole Pia Urio aliwataka wadau kuendelea kuhimiza wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi ili kuwezesha taifa kuondokana na changamoto ya uhaba wa wanasayansi.

No comments:

Post a Comment