Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, December 16, 2014

TANESCO YASEMA MGAWO WA UMEME KUBAKI HISTORIA NCHINI

 Mkurugenzi mtendaji wa Tanesco Mhandisi Felchesmi Mramba akitoa taarifa yaa mikakati ya shirika hilo ili kukomesha tatizo la mgawo wa umeme nchini









 Mkuu wa wilaya ya Mbeya Dk.Norman Sigalla akizungumza na maafisa wa Tanesco kabla ya kufungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa shirika hilo.

 Afisa Mwandamizi wa Tanesco kanda ya Nyanda za juu kusini Salome Kondola akitoa neno la shukrani mara baada ya hotuba ya mkuu wa wilaya 
 Maafisa wa Tanesco wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Mbeya Dk.Norman Sigalla baada ya kiongozi huyo kufungua mkutano wa baraza lao.
 
                            HABARI KAMILI 
 
SHIRIKA la Ugavi la Umeme nchini(Tanesco) limesema ifikapo mwishoni mwa mwaka 2016 Tanzania suala la mgawo wa umeme litabaki kuwa historia.

Uhakika huo unakuja kufuatia mikakati ya utekelezaji wa miradi ikiwemo Kinyerezi namba moja wa megawati 150 ambao hadi sasa asilimia 90 ya utekelezaji wake umekamilika.

Upo pia mradi wa kinyerezi namba mbili wa megawati 240 ambao serikali iko kwenye hatua za mwisho za maelewano ya kifedha baina ya wizara ya fedha,benki ya Japani na benki ya maendeleo ya Afrika kusini ambapo ujenzi wa mradi huo unatarajiwa kuanza mwakani.

Mkurugenzi mtendaji wa Tanesco Mhandisi Felchesmi Mramba ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Baraza kuu la 45 la wafanyakazi wa Tanesco linalofanyika jijini Mbeya.

Mhandisi Mramba amesema miradi ya kinyerezi namba tatu na nne imeanza kwa ubia kwa makampuni mawili ya kichina na utekelezaji wake unatarajiwa kuanza mwakani kama ilivyo kwa kinyerezi namba mbili.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mbeya Dk.Norman Sigalla amewataka watoa huduma kutoka shirika hilo kuwa na lugha zenye kumwelewesha mteja na si kujibu hovyo hovyo.

Dk.Sigalla amesema majibu mabovu ambayo yamekuwa yakitolewa na baadhi ya watendaji wa shirika hilo yamekuwa yakisababisha serikali kulaumiwa na kuonekana haifai kwakuwa haiwathamini wananchi katika kutoa huduma za nishati ya umeme.

Amesema ni vema wataalamu hao wakawa na lugha zenye ukweli kwa wateja badala ya lugha za kuwalaghai na kuwadanganya na mwisho wa siku mteja anakuja kubaini ukweli uliopo na kulichukia shirika na serikali.

No comments:

Post a Comment