Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, December 15, 2014

MWANACHUO TIA ADAIWA KUTUPA KICHANGA DAMPO

Maiti ya mtoto mchanga ikiwa imetelekezwa kama ilivyokutwa na wakazi wa eneo la Airpot jijini Mbeya(Picha kwa hisani ya mmoja wa wakazi wa eneo hilo)

MWANAMKE asiyefahamika ametupa mtoto mchanga katika Dampo la taka lililopo katika eneo la Airpot jijini Mbeya jirani na kilipo chuo cha uhasibu(TIA) tawi la Mbeya.

Wakazi wa maeneo ya jirani na dampo hilo wanasema waliikuta maiti ya kichanga hicho ikiwa imetelekezwa hapo lakini inasadikiwa kuwa kabla ya kutupwa mtoto huyo alikuwa hai.

Hili si tukio la kwanza kwa maiti za vichanga na pia vichanga vilivyo hai kukutwa vimetelekezwa kwenye dampo hili.Baadhi ya wakazi wa maeneo ya jirani na dampo hili wanahusisha matukio ya utupaji watoto wachanga na pia maiti za watoto hao na wanafunzi wa chuo cha TIA.

“Hii si mara ya kwanza kukuta maiti ya kichanga hapa.mara kwa mara tumekuwa tukiokota.Wengi wetu tunaamini wanaofanya ukatili huu ni wanafunzi wanaosoma humo ndani TIA.Wanaagopa kulea ndiyo sababu wanatupa vichanga namna hii” alisema mmoja wa wakazi wa maeneo hayo aliyeomba jina lake kutoandikwa katika Lyamba Lya Mfipa.
 


No comments:

Post a Comment