Maiti ya mtoto mchanga ikiwa imetelekezwa kama ilivyokutwa na wakazi wa eneo la Airpot jijini Mbeya(Picha kwa hisani ya mmoja wa wakazi wa eneo hilo)
MWANAMKE asiyefahamika ametupa mtoto mchanga katika Dampo
la taka lililopo katika eneo la Airpot jijini Mbeya jirani na kilipo chuo cha
uhasibu(TIA) tawi la Mbeya.
Wakazi wa maeneo ya jirani na dampo hilo wanasema
waliikuta maiti ya kichanga hicho ikiwa imetelekezwa hapo lakini inasadikiwa
kuwa kabla ya kutupwa mtoto huyo alikuwa hai.
Hili si tukio la kwanza kwa maiti za vichanga na pia
vichanga vilivyo hai kukutwa vimetelekezwa kwenye dampo hili.Baadhi ya wakazi
wa maeneo ya jirani na dampo hili wanahusisha matukio ya utupaji watoto
wachanga na pia maiti za watoto hao na wanafunzi wa chuo cha TIA.
“Hii si mara ya kwanza kukuta maiti ya kichanga
hapa.mara kwa mara tumekuwa tukiokota.Wengi wetu tunaamini wanaofanya ukatili
huu ni wanafunzi wanaosoma humo ndani TIA.Wanaagopa kulea ndiyo sababu wanatupa
vichanga namna hii” alisema mmoja wa wakazi wa maeneo hayo aliyeomba jina lake kutoandikwa katika Lyamba Lya Mfipa.
No comments:
Post a Comment