JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
Ofisi ya Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa
Mbeya,
Namba ya simu 2502572
S. L. P. 260,
Fax - +255252503734
MBEYA.
E-mail:- rpc.mbeya@tpf.go.tz
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 18.05.2017.
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye
tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana
na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na
wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio
makubwa ya uhalifu.
KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI
[GONGO]
Mnamo tarehe 17.05.2017 majira ya saa
18:00 jioni, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilifanya msako huko katika
kivuko cha Magongo Street, Kata ya Ndandalo, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya
Kyela, Mkoa wa Mbeya na kufanikiwa kuwakamata watu watatu wakiwa na Pombe Moshi
[Gongo] ujazo wa lita 80.
Watuhumiwa
waliokamatwa ni pamoja na:-
1.
AMOS MWAKASAPE
[33]
2.
ROSE D/O ITULO
[35]
3.
TUMAINI MAKULA
[30] wote wakazi wa Tenende Wilaya ya Kyela.
Watuhumiwa walikamatwa
wakiwa wamehifadhi pombe hiyo katika madumu 03 ya lita 20 na vidumu vya lita 5 na chupa zinazokadiriwa kubeba lita 10 kila mmoja. Watuhumiwa walikuwa
wakisafirisha pombe hiyo kwenda kijiji cha Tenende kwa ajili ya kuiuza.
Upelelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika watafikishwa mahakamani.
Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya
limeendelea kukabiliana na matukio makubwa ya uhalifu pamoja na wahalifu. Jitihada
zinaendelea kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha Mkoa wetu unakuwa mahala
salama. Hata hivyo Kumekuwa na tukio 01 la mauaji kama ifuatavyo:-
Mnamo tarehe 17.05.2017 majira ya saa
16:00 jioni huko Kijiji cha Igodima, Kata ya Chokaa, Tarafa ya Kiwanja,
Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya. Mwanaume mmoja ambaye hajafahamika jina lake wala
anuani yake, anaekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 40 - 45, aliuawa na wananchi walioamua kujichukulia sheria
mkononi kwa kumpiga fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia
majeraha yaliyopelekea kifo chake.
Inadaiwa
kuwa, kabla ya tukio hilo marehemu alikuwa amevunja nyumba mchana na kuiba pesa
taslim Tshs 1,500,000/= katika
nyumba ya DANEL KILALA, na wakati
anakimbizwa kwa lengo la kukamatwa alimjeruhi kwa kumchoma kisu cha tumbo DAUDI KILALA [27] Mkazi wa Igodima na ndipo
nae alishambuliwa hadi kuuawa na kundi la wananchi.
Majeruhi
amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chunya
kwa matibabu na mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitalini hapo.
Upelelezi unaendelea.
Mnamo tarehe 16.05.2017 majira ya saa
11:00 Asubuhi huko katika eneo la Iwolelo, lililopo Kitongoji cha Kanoge,
Kijiji cha Kambikatoto, Tarafa ya Kipembawe, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya,
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la NGIKA
NG’WANI [55] Mkazi wa Ipenyelo alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa
Hospitali baada ya kukanyagwa na mnyama pori - Tembo.
Marehemu
alikutana na athari hiyo wakati anatokea eneo la mkusanyiko akiwa anarejea
nyumbani kwake na ndipo alikutana na Tembo ambaye alimkanyaga na kupelekea kifo
chake. Inadaiwa kuwa, marehemu alipoteza maisha kutokana na kutokwa damu
nyingi. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya Chunya.
WITO:
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI anatoa wito kwa wananchi kuacha kutumia
Pombe Haramu ya Moshi kwani ni kinyume cha sheria na ni hatari kwa afya ya
mtumiaji. Pia anatoa wito kwa wananchi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria
mkononi wanapowakamata watuhumiwa kwa tuhuma mbalimbali na badala yake wajenge
tabia ya kuwafikisha katika vyombo vya dola watuhumiwa wanaowakamata kwa makosa
au tuhuma mbalimbali kwa hatua zaidi za kisheria.
Imesainiwa na:
[DHAHIRI A. KIDAVASHARI - DCP]
KAMANDA
WA POLISI MKOA WA MBEYA
No comments:
Post a Comment