Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, May 28, 2017

SIMBA WAPATA AJALI WAKIRUDI DAR ES SALAAM KUTOKA DODOMA






Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa Gari aina ya Land Cruiser iliyokua imebeba wanachama kadhaa wa timu ya Simba na pia Nahodha wa Simba Jonas Gerrard Mkude ikitokea Dodoma kuelekea Dar Es Salaam imepinduka na kuharibika vibaya, maoneo ya Dumila.



Taarifa za awali zinadai kuwa Wanachama hao wa Simba hali zao ni mbaya lakini mmoja wao aliyetajwa kwa jina la Shose anaeonekana katika picha mbili hapo juu amefariki dunia.
Jonas Mkude(katika picha hapo juu) yuko vizuri na yuko na majeruhi wenzake katika hospitali ya mkoa Morogoro wanakoendelea kupata matibabu.


Hao unaowaona katika picha za juu zaidi ni Mashabiki waliokua kwenye Magari Mengine

No comments:

Post a Comment