Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Friday, February 28, 2014

KAIMU AFISA MTENDAJI WA KIJIJI AUAWA KWA KUPIGWA JIWE KICHWANI

MNAMO TAREHE 27.02.2014 MAJIRA YA SAA 01:55HRS HUKO KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA. TITO HANKUGWE (45) KAIMU VEO WA KIJIJI CHA SHASYA ALIFARIKI DUNIA WAKATI ANAPATIWA MATIBABU HOSPITALINI HAPO. MAREHEMU ALIJERUHIWA KWA KUPIGWA JIWE KICHWANI WAKATI ANATOA MSAADA NYUMBANI KWA FURAHA HANKUGWE AMBAYE ALIVAMIWA NA KUNDI LA WATU NANE NA KUBOMOLEWA NYUMBA YAKE PAMOJA NA KAKA YAKE SIKUJUA HANKUGWE TAREHE 26.02.2014 MAJIRA YA SAA 21:45HRS KATIKA KIJIJI CHA SHASYA, KATA YA HALUNGU, TARAFA YA ITAKA. CHANZO CHA TUKIO HILO NI TUHUMA ZA WIZI WA SOLA NA INVETA AMBAPO FURAHA HANKUGWE ALITUHUMIWA KUIBA NYUMBANI KWA MAPINDUZI MAGWAZA MKAZI WA KIJIJI CHA SHASYA. WATUHUMIWA HAO AMBAO WOTE WANAFAHAMIKA WAKIONGOZWA NA AMANI MAGWAZA – MWENYEKITI WA KITONGOJI CHA NAMKWENDE, WENGINE NI MASHAKA BOKO, GIVEN MYOMBE, MAWAZO MAGWAZA, YOHANA MAGWAZA, TULINAO NZOWA, KENETH NGOYA, SIKUJUA NZOWA AMBAO WALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO HILO. JUHUDI ZA KUWATAFUTA WATUHUMIWA HAO ZINAENDELEA. KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI WA POLISI BARAKAEL MASAKI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI WALIPO WATUHUMIWA WA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAO.Taarifa hii ni kwa mujibu wa Kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoani Mbeya Barakael Masaki

No comments:

Post a Comment