Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, February 26, 2014

ZIARA YA RC KANDORO WILAYANI MBARALI

Ziara ilianzia hukoo kata ya Madibira.Kituo cha kwanza kilikuwa shule ya Sekondari Madibira na mkuu wa mkoa akapokelewa kwa kuvishwa skafu na vijana wa Skauti Mkuu wa mkoa akiwa shuleni hapa aliweza kukagua miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Tenki la kuhifadhia maji la chini ya ardhi.Aliweza pia kukagua jengo la maabara kwaajili ya masomo ya sayansi,nyumba ya mwalimu iliyojengwa kisasa na choo kilichojengwa pia kisaa kwaajili ya matumizi ya wanafunzi. Kandoro pia alitembelea mradi wa maji katika kijiji cha Mkunywa.Hapa alikuta hakuna jambo lolote la maana lililokwisha fanyika licha ya mkandarasi kampuni ya JECCS CONSTRUCTION AND SUPPLIERS ya Dar es salaam kulamba zaidi ya milioni 100.Inabainishwa kuwa wafanyakazi wa kampuni hii wamekuwa wakishinda wakilewa pombe eneo la mradi badala ya kufanya kazi hivyo mradi kuendelea kusuasua.Mkuu wa mkoa alionesha kukasirishwa na hatua hiyo ya mradi na kuamuru mkandarasi mshauri kuona uwezekano wa kuishauri halmashauri kuvunja mkataba iwapo mkandarasi ataendelea kusuasua Ziara ikaendelea kwa kukagua miradi mbalimbali na kumalizika siku ya pili katika mradi wa maji wa Igurusi kwa mkuu wa mkoa kukagua Ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji

No comments:

Post a Comment