Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, December 6, 2012

BUNDUKI MBILI ZAKAMATWA MBARALI


SIKU chache baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dk.Emmanuel Nchimbi kutangaza ongezeko la vitendo vya uharifu ikiwemo mauaji ya kutumia silaha na kutoa onyo kwa watanzania wanaomiliki silaha kiholela kuzisalimisha ndani ya siku 30 watu wawili wanashikiliwa na polisi mkoani Mbeya kwa umiliki wa aina hiyo wa silaha.

Miongoni mwa wanaoshikiliwa ambao wote walikamatwa na askari wanyamapori ni pamoja na mwanamke Esther Msigwa(30) mkulima na mkazi wa Kijiji cha Madibira wilayani Mbarali.

Kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa Adam Simfukwe amesema Esther amekamatwa Desemba 5 mwaka huu saa saba mchana na askari wanyamapori waliokuwa doria na kwakuwa mtuhumiwa amekuwa akijihusisha na uwindaji haramu ndipo waliamua kufanya msako nyumbani kwake na kukuta bunduki moja aina ya Gobole aliyokuwa ameificha chumbani kwake.

Katika msako huo pia askari hao wa TANAPA wamemkamata Badede Chafumbo(49) mkazi wa kijiji hicho baada ya kukuta anamiliki gobore moja goroli 41 ambazo hutumika kama risasi na chupa mbili za baruti.

Simfukwe amesema silaha hizo zote zimekuwa zikitumiwa na mtuhumiwa kwa uwindaji haramu katika hifadhi ya Ruaha iliyopo jirani na kijiji cha Madibira jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

No comments:

Post a Comment