Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, December 5, 2012

VIJANA MBALIZI WAJITOLEA KUSAFISHA MIFEREJI ILIYOJAA UDONGO

 Ni kwa kujitolea kama ilivyokuwa enzi za baba wa taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere vijana hawa wa mji mdogo wa Mbalizi wilayani Mbeya wakiwemo wanawake leo hii wameamua kufanya usafi wa mji huo kwa kusafisha mitaro ya maji katika barabara zilizopo jirani na kituo cha mabasi.
 Ni vijana wachache lakini wsalioonekana kuwa na ari ya kutoa somo kwa wenzao kuwa si kila jambo wasubiri serikali ikawafanyie.Waanze wao watakapoishia ndipo serikali kupitia halmashauri iende kusaidia
 Mbunge wa jimbo la Mbeya(Kulia) mchungaji Luckson Mwanjala akavutiwa na kazi ya vijana hao alipopata taarifa na kuamua kufika eneo la tukio kujionea
 Mwanjala akavutiwa na kazi ya vijana hao na kuamua kutoa shilingi 150,000 zisaidia kununua vinywaji baridi wakati vijana wakiendelea na shughuli hiyo

 Mbunge akaondoka na kuacha vijana wakiendelea na kazi hiyo ikiwa ni siku ya kwanza ambapo kesho wataendelea.Lakini ni kazi ambayo vijana hawa wanasema haihusishi hata kidogo itikadi za kisiasa bali maendeleo ya eneo lao.
 Kuna wakati ililazimu nguvu ya ziada itumike ili kurahisisha usafishaji wa mitaro iliyoziba.Hapa ni daraja dogo ambalo lazima lizibuliwe lakini ili kufanya hivyo lazima pia kuondoakaravati za zege na saruji.

Mratibu wa shughuli ya kujitolea kwa vijana hao Godorn Kalulunga hakuwa nyuma kuonyesha mfani kwa kufanya kazi kama anavyoonekana katika picha hii juu.
Baada ya kazi ya siku ya kwanza ikawalazimu vijana kukaa kujadiliana nini kitafanyika kesho alhamisi

No comments:

Post a Comment