WAHAMIAJI haramu 28 wote raia wa Ethiopia wanashikiliwa na jeshi la
polisi mkoani Mbeya kwa kuingia nchini kinyume cha sheria.
Kadhalika jeshi hilo linamshikilia dreva taxi aliyefahamika kwa jina la
Christopher Alfred(39) mkazi wa Veta jijini Mbeya kutokana na wahamiaji hao
haramu kukutwa katika pagala la nyumba yake anayoendelea kuijenga.
Kaimu kamanda wa polisi mkoani hapa Adam Simfukwe amesema kuwa wahabeshi
hao wamekamatwa na askari waliokuwa doria desemba 5 mwaka huu majira ya saa 4:00 usiku katika eneo la Veta jijini Mbeya.
Simfukwe amesema watuhumiwa wakiongozwa na mwenzao aliyefahamika kwa jina
la Mohamed Kabebe(27) walikuwa wamejificha ndani ya pagala hilo lakini
haikufahamika mara moja waliingia jijini hapa wakitokea wapi na ni wapi
wanakoelekea.
Amesema taratibu za kisheria zinaendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na
kuwakabidhi wahamiaji hao kwa Idara ya Uhamiaji ili iendelee na mchakato
mwingine wa kisheria dhidi yao.
No comments:
Post a Comment