Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, November 24, 2013

WANAHABARI JOACHIM NYAMBO NA VENANCE MATINYA WAIBUKA MABINGWA WA KUPANDA MLIMA MBEYA

Haikuwa kazi rahisi kuufikia msalaba huu uliopo katika safu ya mlima Mbeya.Kilichokuwa kiikitutisha zaidi ni wingu zito lililotanda mara tu baada ya sisi kufika msalabani hapa.Hofu ya kunyeshewa na mvua ikawa mioyoni mwetu.Lakini tulipiga magoti na kumwomba mwenyezi Mungu.Naama sala zetu zikarsikika maada ya manyunyu kidogo wingu hili unaloliona hapa juu likasambaa Mwandishi wa gazeti la Jamboleo Venance Matinya akifurahia kufika katika msalaba huu kabla ya kuendelea na safari ya kupanda mlima hadi ilipo minara ya vituo mbalimbali vya mawasiliano Mwonekano wa jiji la Mbeya ukiwa katika eneo la msalaba mlimani Safari ikaendelea kutoka eneo la msalama na kupanda zaidi mlima hadi kilele kikuu na baadaye kushukia katika kijiji cha Mbeya Peack kabla ya kushuka mlima huo kurejea jijini Mbeya Kuna wakati ilibidi kupumzika kwa muda kama anavyoonekana mwandishi Venance Matinya akiwa hoi na kuliona jiwe hili kama mkombozi kwake kwakuwa maeneo mengine ni vigumu kukaa kwani ungeweza kuhisi kizunguzungu. SAFARI HII IMEFANYIKA JUMAPILI HII AMBAPO WANAHABARI VENANCE MATINYA NA JOACHIM NYAMBO WALIIBUKA MASHUJAA WA KUPANDA MLIMA MBEYA BAADA YA WADAU WENGINE KUINGIA MITINI.

No comments:

Post a Comment