Wadau mbalimbali waliohudhuria mdahalo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika wakitokea katika kata za Ilembo na Masoko wilayani Mbeya wakiwa kwenye piacha ya pamoja.
Mratibu wa GBV na
VAC Patrick Kossima akiimba na kucheza na wanafunzi waliohudhuria mdahalo kijijini Ilembo
Mwanafunzi Sylivia Lugano akichangia mada kwenye mdahalo huo ulioandaliwa na kanisa la Anglikana kupitia mradi wa GBV na VAC unaofadhiriwa na shirika la Watereed.
Afisa mtendaji wa kata ya Masoko Joseph Lupama akizungumza jambo kwenye mdahalo.
Mratibu wa GBV na
VAC Patrick Kossima akitoa zawadi kama motisha kwa wanafunzi waliowahi kufanya vizuri katika masomo yao shuleni wakapewa zawadi na shule lakini wazazi hawakuwapa zawadi wakati huo
WAZAZI na walezi wilayani Mbeya
wametajwa kuwa hufurahia mno pale watoto wao wanaposimamishwa masomo shuleni
kwa kutolipa michango wakijua ni wakati muafaka wa kuwatumikisha watoto hao
katika shughuli mbalimbali zikiwemo kilimo.
Tabia hiyo ya wazazi imetajwa kuwa
kikwazo kikubwa katika ustawi wa taaluma ya watoto wilayani hapa hali inayozua
changamoto kwa wadau wa maendeleo kuona umuhimu wa kuingilia kati ili kuinusuri
jamii ya watoto wilayani hapa.
Wanafunzi,walimu na wazazi kutoka
kata za Ilembo na Masoko wilayani Mbeya walibainisha kuwepo kwa hali hiyo
kwenye mjadala wa pamoja ulioandaliwa na Kanisa la Anglikana kupitia mradi wa
Kupinga Ukatili wa kijinsia(GBV) na ukatili dhidi ya watoto(VAC) ikiwa ni
katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika.
Wadau hao walisema kutokana na
uelewa mdogo juu ya umuhimu wa elimu,wazazi wengi wamekuwa wakiwanyima fursa
watoto wao kwenda shule na badala yake kuwatumikisha mashambani wakiamini kuwa
kilimo kina manufaa makubwa ndani ya familia zaidi ya Elimu.
Walisema kutokana na uelewa huo
mdogo wazazi hupuuzia sula la kulipa michango mbalimbali wakisubiri uamuzi wa
uongozi wa shule kuwasimamisha kwa muda wanafunzi na hapo ndipo wazazi na
walezi hao hufurahia kwakuwa hupata sababu ya kuendelea kuwatumikisha watoto
mashambani.
“Unapofukuzwa shule kwakuwa hujatoa
mchango na kurudi kwa mzazi,mzazi anakwambi hakuna pesa nenda shambani kwani
shule inakusaidia nini.Kwao inakuwa ni sherehe lakini wanasahau kuwa tunakosa
haki yetu ya msingi” alisema mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya
msingi Ilembo Jemedari Ezekiel.
“Hata unapokwenda kumuomba mzazi
daftari au kalamu jambo la kwanza atakwambia kwanza ukafanye kazi shambani
kwake au kwa jirani ili pesa utakayolipwa ndiyo ukanunue mahitaji yako”
aliongeza Jemedari.
Nao wali Gabriel Mwandembo kutoka
shule ya msingi Mumba na Valina Kamumyana wa shule ya sekondari Ilembo walisema
ushiriki mdogo wa wazazi katika kufuatilia taaluma ya mwanafunzi umekuwa
ukisababisha watoto wengi kwenda shule kwa lengo la kuhitimu tu darasa la saba
na si kupata elimu ya kumsaidia maishani mwake.
Kwa upande wake mratibu wa GBV na
VAC Patrick Kossima alisema mijadala zaidi inahitajika ndani ya jamii ili
kuwezesha kupanua wigo wa uelewa kwa wazazi hatua itakayosababisha kila upande
kutambua wajibu wake na kuijenga jaii yenye upendo.
Kossima alisema kasoro zilizopo ndani ya jamii
katika malezi ya mtoto ni miongoni mwa mambo yanayosababisha uwepo wa
maambukizi mapya ya Virusi vya ukimwi japo ni wanajamii wachache wanaotambua
jambo hilo.
No comments:
Post a Comment