Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, June 1, 2015

PROF MARK MWANDOSYA ATANGAZA NIA RASMI KUWANIA URAIS 2015



 Waziri wa nchi ofisi ya rais Prof Mark Mwandosya akizungumza na wakazi wa mkoani Mbeya kwenye viunga vya ukumbi wa Benjamini Mkapa jijini Mbeya jana alipotangaza nia ya kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM).








Viongozi wa jadi wakifuatilia kwa karibu sherehe za kutangaza nia..






WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais Prof Mark Mwandosya leo ametanga nia ya kuwania nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) huku akisema yeye si bingwa wa kujisifia kama wanavyofanya wengine.

Prof Mwandosya ambaye alivitumia viwanja vya Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo Sokomatola jijini Mbeya,viwanja ambavyo ndivyo vilitumika kwenyemikutano ya Mwalimu Julias Nyerere alipokuwa akihamasisha harakati za kutaka uhuru wa Tanganyika alisema hana alichofanya yeye kama yeye bali yapo mengi aliyoyafanya kwa kushirikiana na wadau wengine.

Akizungumzia vipaumbele vyake,Prof Mwandosya alisema katika elimu angependa kuona elimu ya msingi inakuwa ya kuanzia darasa la kwanza hadi kiidato cha nne huku pia akisisitiza umuhimu wa jamii ya wanawake kupewa kipaumbele katika kupewa elimu.

Kwa upande wa Sekta ya afya alisema kwa muda mrefu taifa limejikita katika kutenga bajeti kubwa kwaajili ya matibabu badala ya kuwekeza kwenye mikakati ya kinga jambo ambalo litawezesha serikali kuepukana na gharama kubwa.

Alisema ni wakati kwa serikali kuhakikisha kila mdau wa sekta ya afya anawajibika ipasavyo kwa kuiwezeshya jamii kujikinga na maradhi badala ya kuhangaikia matokeo ya maradhi.

Akizungumzia suala la amani na utulivu alisema ni jambo la msingi kwa jamii kuendelea kutambua kuwa Amani na utulivu uliopo nchini ni tunu pekee kutoka kwa Mwenyezi Mnungu hivyo walinzi wa kweli wanapaswa kuwa wao japo kuna haja pia ya kuendelea kuimarisha vikosi vya ulinzi na usalama.

„Kwa upande wa ajira kwa vijana,bado tuna changamoto,lakini hii ni kutokana na vijana wengi kuwa na mawazo ya kuajiriwa zaidi kuliko kujiajiri.Tunapaswa kufikiri zaidi na kuondokana na dhana ya kuuza vyetu badala ya mawazo na dehamira mpya.Ni muhimu tukahamasioka hata kuvuka mipaka ya nchi yetu.hii itatuwezesha kupata fedha nyingi kwa kuwa na watanzania wanaofanya shughuli zao nje ya nchi”.

Waziri huyo pia aliwatupia lawama baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakienda nje ya nchi na kwenda kutoa matamko yenye kuisema vibaya nchi yao hatua aliyosema ni ya kusononesha na haitofautiani na watanzania wengine ambao uzalendo kwa nchi yao umepungua katika kuipenda nchi yao,kutothamini vitu vinavyozalishwa nchini sambamba na kutoipenda lugha yao ya taifa yaani Kiswahili.

Katika hafla hiyo ya kutangaza nia,wakazi mkoani hapa walimchangia Prof Mwandosya zaidi ya shilingi milioni 10.7 kwaajili ya kuchukulia fomu ya kugombea urais ambapo waziri huyo alisema atachukua fomu hiyo jumatano hii mjini Dodoma.

Awali mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya siasa mkoani Mbeya Godfray Mwandulusya alisema vyama vya upinzani mkoani hapa viko pamoja na Prof Mwandosya kutokana na historia yake isiyomuonesha kuwa mtu mwenye kashfa katika nafasi alizowahi kuzitumikia.

Kwa upande wake mwakilishi wa viongozi wa kimila mkoani hapa Chifu Soja Masoko alisema kiongozi anayehitajika wakati huu ni yule asiye na nia ya kuwagawa watanzania badala ya kuwaunganisha.

No comments:

Post a Comment