Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Saturday, June 13, 2015

JANUARY MAKAMBA-MBIO ZA KIJITI ANAPEWA MWENYE NGUVU,HAPEWI ALIYECHOKA




January Makamba akiwapungia mkono wananchi na wanachama wa CCM mkoa wa Mbeya wakati akishuka kutoka garini, wananchi hao walifika hapo katika ofisi za CCM wila ya Mbeya Mjini kwa aijili ya kumdhamini.

Katibu wa CCM wliaya ya Mbeya Mjini, Kurwa Milonge akimkabidhi January Makamba fomu yenye majina na sahihi za wanachama wa CCM waliomdhamini

January Makamba akihutubia wanachi na wanachama wa CCM mkoani Mbeya  mara baada ya kukabidhiwa fomu yenye majina na sahihi za wanachama waliomdhamini


January Makamba akiweka sahihi katika kitabu cha wageni katika ofisi ya katibu wa CCM wilaya ya Mbeya Mjini mara baada ya kuwasili katika ofisihizo, kushoto ni mkewe Ramona Makamba

 
January Makamba na mkewe, Ramona Makamba wakiwapungia mikono wananchi na wanachama wa CCM mkoa wa Mbeya  walipowasili katika viwanja vya ofisi za CCM wila ya Mbeya Mjini
                             HABARI KAMILI
NAIBU waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia January Makamba amepata wadhamini 1678 katika viunga vya ofisi ya CCM mkoa wa Mbeya leo.

Akiwa mkoani Mbeya Makamba licha ya kuponda makada wengine ndani ya chama hicho akiwalaumu kuwa wanatumia fursa ya kuwapaka matope makada wengine waliotangaza nia na kuchukua fomu yeye amesema mfumo wa mbio za kijiti ni aliyechoka kukimbiza kumpa aliye na nguvu ili akimbize zaidi.

Amesema hatarajii kuona CCM inatoa kijiti kutoka kwa mtu aliyechoka na kumpa mkimbizaji aliyechoka bali itampa kijiti hicho mkimbiaji mpya na mwenye nguvu za kutosha kumudu kasi ya mashindano ili kufikia malengo ya ushindi.

Amesema kwa sasa CCM inapaswa kutambua kuwa wakati uliopo ni wa kukabidhi madaraka kwa uongozi wa kisasa unaoendana na mambo ya kisasa yaliyopo badala ya kuendelea kuuacha kwa kizazi kisichoendana na kasi iliyopo hali inayoweza kuzorotesha ustawi wa kizazi chote.

No comments:

Post a Comment