Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, June 3, 2015

UNICEF YAZINDUA MPANGO WA KUOKOA MAISHA YA MAMA NA MTOTO MKOANI MBEYA



 Meneja wa Afya wa Unicef kutoka Dar es salaam Dkt.Tadashi Yasuda akielezea Visababishi vya vifo vya wajawazito na watoto wachanga alipowasilisha mada ya mradi kwa mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro na wageni wengine.
Mwakilishi wa shirika la KOICA nchini Seung Kim akibainisha namna shirika hilo lililodhamiria kusaidia katika kutekeleza mpango huu na namna fedha zilivyopatikana
 Wajumbe wakiwemo wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri na wanakamati za afya za wilaya wakifuatilia hotuba ya mkuu wa mkoa.


 Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akihutubia wajumbe waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa mpango huu


Diwani wa kata ya Isanga jijini Mbeya Shekhe Dull Mohamed akitoa neno la shukrani.Ni baada ya mkuu wa mkoa kuzindua.


                          HABARI KAMILI
SHIRIKA la kusaidia watoto Duniani(Unicef) limetaja mambo matatu makuu yanasosababisha vifo vya wanawake wajawazino na watoto wachanga nchini na kubainisha kuwa iwapo jitihada za dhati hazitafanyika kukabiliana na mambo hayo harakati za kupunguza vifo hivyo haziwezi kuzaa matunda.



Meneja wa Afya wa Unicef kutoka Dar es salaam Dkt.Tadashi Yasuda ameyataja mambo hayo kuwa ni Kuchelewa kuchukuliwa kwa maamuzi ya mama mjamzito kwenye vituo vya huduma za afya,Ukosefu wa miundombinu ya uhakika ya usafiri na pia Hali ya utoaji huduma isiyoridhisha.



Katika hafla fupi ya uzinduzi wa mpango wa miaka minne wa Kusaidia maisha ya Akina mama na Watoto kwa halmashauri 10 za mkoani hapa unaofadhiliwa na shirika la Korea International Cooperation Agency(KOICA) kupitia Unicef Meneja huyo amesema changamoto hizo ni chanzo kikubwa cha vifo nchini.



Amesema katika kaya nyingi nchini maamuzi ya kumpeleka wanafamilia kwenye vituo vya tiba hutegemeana na wanaume jambo ambalo husababisha wajawazito wengi kuchelewa kufikishwa kwenye maeneo hayo na kupewa huduma stahili.



Amesema pia changamoto ya Usafiri inayotokana na ama uhaba wa vyombo vya usafiri au ubovu wa miundombinu imekuwa ikikwamisha wajawazito na watoto wachanga kufikishwa kwa wakati kwenye vituo vya tiba na wanapofikishwa tayari wanakuwa katika hali mbaya.



Meneja huo amesema hali ya utoaji huduma isiyoridhisha kwenye vituo vya tiba ni changamoto nyingine ambayo hutokana ama na watoa huduma kutoijali kazi yao au uhaba wa rasilimali watu na vitendea kazi.



Kwa upande wake mkurugenzi wa Afya na Lishe wa Unicef Dkt.Sudha Shema ameshauri halmashauri zilizofikiwa na msaada wa mpango huo kuweka mikakati ya dhati yenye kuwezesha kupunguza changamoto kwenye sekta za afya ili kuendana na malengo ya milenia.


Akizungumzia mpango huo,mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro ametaka wadau wa sekta ya afya mkoani hapa kutowaachia watu wachache kutekeleza mradi husika badala yake kila mmoja awajibike kwa nafasi yake.

No comments:

Post a Comment