WATU wanane
wamefikishwa na kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya
Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi kujibu shitaka la
kumjeruhi kwa mapanga na kisha kumkata mkono na kutomomea nao
wa mwanamke mmoja aitwaye Remi Luchumi (30) mkazi
wa Mwamachoma Tarafa ya Mamba Wilaya ya Mlele na kisha kutokomea
nao.
Watuhumiwa hao walipandishwa kizimbani hapo
jana mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa
Katavi Odira Amworo.
Washitakiwa hao nane
waliopandishwa kizimbani ni Alex Manyanza (24) Nogele
Maliganya (Hombohombo) 40 Galula Nkuba(45) Shile
Jilala(27) Masunga Kashinje(34) Maiku Punga (27)
Koga Silanga(32) wote wakazi wa Kijiji cha Maji moto Tarafa ya Mamba
Wilaya ya Mlele na Salumu sawa Mkazi wa Meatu Shinyanga.
Mwendesha mashita
mwanasheria wa Serikali wa Mkoa wa Katavi Hongera Mwakifimbo alidai
mahakamani hapo kuwa, watuhumiwa walitenda kosa hilo
hapo Mei 14 mwaka huu nyakati za saa sita usiku nyumbani kwa wazazi
wake na Albino huyo katika Kijiji cha Mwamachoma.
Watuhumiwa wanadaiwa kwamba
siku hiyo ya tukio walikwenda nyumbani kwao na Remi
Luchoma na walimkuta akiwa amelala na kisha walimjeruhi kwa mapanga
sehemu ya mkono wake na kisha walifanikiwa kumkata kingaja cha mkono wake
na kisha walitokomea nacho
Baada ya kusomewa
mashita na mwanasheria wa serikali Mawiti Malifimbo katika
kesi hiyo ambayo ilimevutia hisia za watu wengi wa Mkoa wa Katavi.
Washitakiwa wote kwa
pamoja walikana kutenda kosa hilo na
waliomba Mahakama iwape dhamana kwa kuwa walikuwa na watu wa kuwadhani.
Hata hivyo
maombi hayo yalipigwa vikali kwa kile kilichodaiwa na mwanasheria wa Serikali
kuwa endapo washitakiwa watapewa dhamana wanaweza kuharibu ushahidi kwani
bado kuna watuhumiwa wengine wanaendelea kutafutwa.
Hakimu
Odira baada ya kusikiliza maombi ya pande hizo mbili aliamuru
washitakiwa wapelekwe rumande hadi hapo Julai 15 ambapo kesi hiyo
itakapo tajwa tena.
Tukio la kukatwa kwa mkono
kwa Albino huyo limekuwa ni la kwanza kutokea katika Mkoa wa Katavi
tangia kuanza kutokea kwa mauaji ya Albino hapa nchini
KWA HISANI YA BLOGU YA PEMBEZONI KABISA.
KWA HISANI YA BLOGU YA PEMBEZONI KABISA.
No comments:
Post a Comment