MWENYEKITI wa
halmashauri ya wilaya ya Mbeya Anderson Kabenga ametangaza kuwania nafasi ya
ubunge Mbeya vijijini kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) kwenye uchaguzi ujao.
Kabenga maarufu kama
Ndombolo ya Solo ametangaza nia ya kuwania nafasi hiyo alipozungumza na Lyamba Lya Mfipa jijini Mbeya ambapo ameweka wazi kuwa kipindi alichokaa katika
madaraka ya udiwani kwa miaka kumi ikiwemo mitano aliyoshika uenyekiti wa
halmashauri kinatosha na sasa anataka ubunge.
Hata hivyo Kabenga
hakuweka bayana kuwa kunuia kwake kuukwaa ubunge kunatokana na mbunge wa Sasa Luckson
Mwanjale kushindwa kuwatumikia wananchi wa jimbo hilo,badala yake alisema yapo
mambo anayoona hayaendi sawa na kwa nafasi ya uenyekiti anashindwa kuyafanyia
kazi.
Mwenyekiti huyo amesema
miongoni mwa mambo yanayomsukuma kuwania nafasi hiyo ni kuvalia njua jukumu la
kuipigia debe bajeti inayopitishwa na halmashauri atakapokuwa bungeni akisema
kwa sasa kuna kusuasua katika kuipitisha bajeti inapofika kwenye ngazi ya
bunge.
Akizungumzia mafanikio
yaliyopatikana katika kipindi cha uongozi wake kwenye halmashauri,amesema
kupatikana kwa hati safi kutoka kwa mkaguzi na msimamizi wa hesabu za serikali(CAG)
ni sehemu ya mafanikio ya kujivunia.
Kabenga pia amewataka
wananchi kuwapuuza watu wachache aliosema wanajariobu kumchafua kwa kumtaja
kuwa mmoja wa wafuasi wa wagombea wa nafasi ya urais wanaotumia fedha nyingi
kuwarubuni wananchi akisema malengo yake ni kuwatumikia wananchi kwa uadilifu
na si kusaka utajiri.
No comments:
Post a Comment