Ndugu Wasamaria wema
Napenda kutumia fursa hii kukushirikisha
habari ya kusikitisha kuhusu dada Joyce Mwambepo (pichani akiwa na mwanaye, na
migu yake iliyopooza) mkaazi wa Sinde jijini Mbeya. Dada huyu mwenye umri wa
miaka 27 anaishi na bibi yake mwenye umri wa miaka 80 pamoja na mwanaye mwenye
umri wa miaka 4.
Kwa bahati mbaya mwezi April mwaka jana dada
huyu alipata ajali ya kugongwa na gari ambayo haikusimama kumsaidia. Ila kwa
msaada wa wasamaria wema alipelekwa hospitali ya
rufaa ya mkoa wa Mbeya ambako inasemekana alikaa kwa miezi mitatu bila kupata
matibabu.
Katika uchunguzi wa awali ilibainika kuwa
Joyce amevunjika miguu yote miwili, hivyo akahamishiwa katika hospitali ya
Taifa Muhimbili ambako pia baada ya kukaa kwa miezi kadhaa alirejeshwa Mbeya
baada ya kukosa shilingi 550,000/- za vipimo na matibabu.
Hadi nakutana naye dada huyu alikuwa amelala
nyumbani kwa bibi yake (pichani kushoto) ambaye ni mlezi wake tangu akiwa na
miaka minne baada ya wazazi wote wawili kufariki dunia.
Hawezi kukaa wala kusimama na anajisaidia
hapo hapo kitandani kwa msaada wa mwanaye na bibi yake. Inasikitisha.
Hivyo nimejitahidi kufuatialia ili kujua
mahitaji halisi lakini sikufanikiwa kumpata daktari bingwa wa mifupa . Ili
kumsaidia Joyce inatakiwa aanze process upya za matibabu kuanzia hapa Mbeya
referral Hospital hadi Muhimbili jijini Dar es salaam.
Gharama za matibabu ni kama ifuatavyo:
1. shilingi 300,000/- za kupima CT-SCAN
2. Shilingi 250,000/- za MRI
3. Usafiri wa kutoka Mbeya-Dar kwa gari
maalum la kukodi 700,000/-
4. Gharama za msaidizi ambaye ni rafiki yake
300,000/-
5. Chakula 450,000/- (Endapo watakaa
hospitali mwezi mzima)
6. Gharama za matibabu (CT-SCAN&MRI ni
vipimo tu) 500,000/-
7. Na mahitaji mengineyo wakiendelea kupata
tiba 500,000/-
Hivyo kwa kuanzia kiasi cha shilingi
3,000,000/- (milioni tatu) kinahitajika kumpunguzia mateso dada yetu huyu.
Asante sana kwa moyo wako wa kujitoa na Mungu atakubariki.
Deo Kakuru Msimu
Msamaria mwema
+255769 512 420
No comments:
Post a Comment