Na Joachim Nyambo.
AMA hakika tasnia ya filamu mkoani Mbeya inaonesha
kuzidi kushika kasi na kulifanya jiji hilo kuwa miongoni mwa miji mikubwa nchini
yenye wasanii wanaofanya kazi zinazohitaji pongezi.Nalizungumza hili baada ya
kuona jitihada zinazofanywa na wacheza filamu wa mkoani hapa.Kazi wanazofanya
kwa sasa ni tofauti kabisa na walizofanya miaka kadhaa iliyopita huko nyuma.
Napata jeuri ya kuyasema haya kwakuwa na ushahidi wa
filamu ambayo hivi sasa imelitenga soko la filamu nchini kote.Hii ni filamu ijulikanayo
kwa jila la Priscar.Filamu hii imeandaliwa na kuchezwa na wasanii wa Mbeya
kupitia kampuni ya Orange filim Entertainment yenye maskani yake jijini Mbeya.
Washiriki wakuu katika filamu ya Priscar ni pamoja
na Mwanadada Jackline Charles aliyebeba jina la filamu.Msanii huyu ambaye mwaka
jana alitamba vizuri katika filamu ya Vanilla iliyochezwa pia na wasanini
wakazi wa jijini Mbeya ameonesha kuiva zaidi kwenye filamu ya Priscar.
Washiriki wengine ni Andrew Mlelema(Hansi),Ally
Abdul-(Daniel) na Aisha Omary(Doreen).Hawa kwa pamoja wamefanya kazi kubwa ya
kuifanya filmu ya Priscar kusheheni kila aina ya burudani kwa wapenzi wa filamu
na pia mafunzo kulingana na maisha ya mwanadamu.
Priscar ni filamu ya kwanza kutengenezwa na kampuni
ya Orange filim Entertainment.Stori yake iliandaliwa na Andrew Mlelema ambaye
pia ni miongoni mwa walioshiriki kucheza na skripti ikaandaliwa na Takesh Edward.
Pamoja na burudani iliyopo ndani ya filamu hii,yapo
mafundisho mbalimbali unayoweza kuyapata baada ya kuitazama.Fundisho la kwanza
ni pale inapoonekana haraka na tama vinavyoweza kumharibia mwanadamu mfumo
halali wa maisha na kujikuta akiingia katika maisha mengine yasiyo endelevu
kwake japo kwa muda mfupi yanaweza kuonekana ni mazuri.
Mfano mzuri wa fundisho hili ni pale ambapo Priscar
baada ya kumuomba kwa siku kadhaa mchumba wake Daniel pesa kwaajili ya kulipia
matibabu ya shangazi yake aliyelazwa hospitalini.Kwakuwa ilikuwa katikati ya
mwezi Daniel hakuweza kupata fedha kwa wakati na ikamlazimu kuendelea kumuomba
mchumba wake kuvuta subira kwakuwa anajaribu kila sehemu kukopa inashindikana.
Hapo Priscar alifikia hatua ya kuamini mchumba wake
hataki kumsaidia na akaamua kutafuta njia nyingine kupata fedha kwaajili ya
kulipia matibabu ya shangazi.Hapo ndipo alipojikuta anaangukia katika mikono ya
kijana Hansi mmiliki wa kampuni ya kutoa mikopo ya fedha.Prisca baada ya
kusaidiwa fedha na milionea Hansi akajikuta anajitumbukiza katika penzi na
tajiri huyo na kumwacha Daniel akihaha asijue la kufanya.
Lakini maisha ya kuponda raha na starehe kati ya
Priscar na mchumba mpya Hansi yakafikia tamati baada ya mrembo huyu kubaini
kuwa kijana huyo ana mchumba wa siku nyingi na haina ubishi kuwa anampenda
zaidi yake na wako mbioni kuoana.Hapo ndipo Priscar akajikuta njia panda kwani
hata alipomkumbuka mchumba wa awali,akakuta tayari Daniel alikwishapata mchumba
mwingine na ni mjamzito.
Fundisho la pili ni namna binadamu wasivyopaswa
kuishi kwa kudharau watu wasiowajua.Hili linajitokeza katika kipande ambacho
kinamuonesha Mrembo Priscar akiwa kituo cha mabasi kusubili daladala,mara
anapita kijana Hansi na kumbembeleza kumpa rifti.Kwa kujiona mrembo na mwenye
hadhi kuliko anayembembeleza Priscar alionesha dharau hapa pale alipokubali
kupanda kwenye gari mpaka aliposhushwa.
Kwa bahati mbaya safari ya Priscar ilikuwa ni kwenda
kufuatilia maombi ya mkopo aliyokuwa amepeleka katika kampuni moja.Kwakuwa fomu
zake za maombi ya mkopo hazikukamilika alishauriwa na watoa huduma kwenye ofisi
hizo aende kuonana na mkurugenzi wa kampuni ili aone uwezekano wa kumsaidia.
Hamadi!bosi ndiye Yule kijana aliyeoneshewa dharau
njia nzima alipojitolea kumpa rifti mrembo Priscar.Huo ndiyo ukawa mwanzo wa
Priscar kujutia dharau zake kwa mtu asiyemjua.
Lipo fundisho la tatu.Hili ni wanadamu kutodharau
watu wanaofanya shughuli flani na kuwaona makahaba au watu wanaojiuza na
wasioweza kuishi maisha yenye mfumo unaostahili hususani wahudumu kwenye
baa.Hili linajitokeza pale kijana Daniel anapoonesha kukerwa na ushauri wa
rafiki yake Jackob anayemshauri kwakuwa Priscar amemsaliti basi asipate shida
achukue japo mhudumu mmoja pale baa walipokaa ili akamliwaze.
Hapo ndipo Daniel anaonesha kuwa anachokiamini yeye
ni kila mhudumu wa baa ni kahaba.Anasema hawezi kuwa na mwanamke anayefanyakazi
baa.Lakini baada ya kufukuzwa kazi kutokana na kupoteza majalada aliyoagizwa na
bosi wake,Daniel anajikuta anaangukia mikononi mwa mhudumu aliyemwokoa siku
alipolewa zaidi pombe na kuamua kumlaza katika chumba cha wahudumu wa baa.
Kwa kuyumba kimaisha Daniel akalazimika kuishi na
mhudumu huyo na hatimaye kumpa ujauzito.Mhudumu huyu anaonesha hali ya kumjali
Daniel na kumfariji kila wakati hasa pale anaporudi akiwa mchovu kutokana na
shughuli ya kuzurula mjini kusaka ajira mpya.Anaendelea kumjali mpaka siku
aliporejeshwa kazi baada ya majalada yaliyopotea kupatikana.Hapo Daniel
akaamini kuwa amepata mchumba mwema zaidi ya Priscar japo mchumba wa sasa
walikutana baa.
Waandaaji wanasema zipo changamoto nyingi
zilizoukabili mchakato mzima wa uandaaji wa filamu ya Priscar iliyorekodiwa na
kampuni ya S Media ya mkoani Morogoro.Moja ya changamoto kubwa ilikuwa ni
kupotea kwa kazi ya kwanza baada ya kutoka location.
“Kazi ilipotea kwenye Extenal disc.Ilitupa wakati
mgumu kwani ilitubidi kujipanga kuanza kazi upya.Ilikuwa Februari mwaka jana
ambapo kazi ilipotea katika mazingira ya kutatanisha.Lakini tulijipa moyo
tukarudi Locationi kufanya upya” anasema mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Orange
filim Entertainment Andrew Mlemela.
“Tumetumia takribani miaka miwili mpaka kuja
kuikamilisha filamu na kuiingiza sokoni.Kwakuwa ni filamu yetu ya kwanza
hatukuona haja ya kutumia wasanii walio na majina makubwa.Tulitaka tufanye
wenyewe ili tujipime na pia wadau watupime.Ndiyo sababu tulishirikisha pia wadu
kwa kila hatu tuliyofikia”.
Anasema wadau wengi wa filamu waliyoitazama
wanaonesha kuridhishwa nayo.Huo ni mwanzo mzuri kwa kampuni kujipanga kwa kazi
nyingine nyingi zaidi na zenye ubora unaohitajika.Japo wanatishwa na utitiri wa
filamu sokoni.
Anasema sanaa ya filamu kwa mikoa ya kanda ya nyanda
za juu kusini inakwamishwa na baadhi ya waandaaji wasiozingatia umakini katika
utekelezaji wa majukumu yao.
No comments:
Post a Comment