Mzaramo alitangaza anatibu
magonjwa yooooooote kwa tsh. 100,000/= Na kama akishindwa kukutibu
anakurudishia laki yako nakukuongeza laki nyingine. MCHAGA akaona hii fursa
yakujipatia hela aiwezi mpita akaenda kutibiwa.
MZARAMO: "unaumwa nini?"
MCHAGA: "Sisikii ladha ya aina yoyote mdomoni kabisaaaa.."
MZARAMO:
"sawa, toa laki kabisa.." Mchaga akatoa.
MZARAMO akamuagiza msaidizi
wake; "Naomba kikopo no.27 mpe anywe huyu.."
MCHAGA akanywa akatema
faster; "Puh puu puu, Aisee huu si mkojo
huu..?"
MZARAMO: "Umepona karibu tena.." Mchaga aka-mind sana
Kesho yake akarudi tena hakuamini ameliwa pesa
yake. MCHAGA: aisee nina tatizo la kumbukumbu nasahau sanaaaaa.." MZARAMO
akamwambia "hakuna tabu, toa laki tukupe tiba..' MCHAGA akatoa pesa akijua
leo lazima afanikiwe..'
MZARAMO: "nesi naomba kikopo no.27.."
MCHAGA:
"ASA CHALII ANGU HICHO SI CHA JANA CHA MKOJO HICHO AISEE..?"
MZARAMO:
"UMEPONA KUMBUKUMBU UNAYO.
No comments:
Post a Comment