Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, November 16, 2015

MTANILA WANASUBIRI UMEME KWA HAMU KUBWA

WAKAZI wa vijiji vilivyopo katika kata ya Mtanila wilayani Chunya wameonesha nia ya kweli ya mahitaji ya umeme wakisema wamejiandaa kunufaika nao mara tu utakapofikishwa kijijini hapo.

Tayari serikali kupitia wakala wa Umeme vijijini(Rea) imefikisha nyaya za umeme kwenye vijiji vya kata hiyo na kuna kila dalili za nishati hiyo kuanza kugawanywa kwa wananchi hivi karibuni.


Miongoni mwa vijiji vilivyofungiwa tayari nyaya za umeme ni Igangwa ambapo wakazi wake wanasema hivi sasa wanaomba usiku na mchana shughuli za ufungaji huo zikamilike mapema ili waanze kunufaika kama ilivyo kwa maeneo mengine nchini.

Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Igangwa Hamis Mwandura alimwambia mwandishji wetu kuwa wakazi wana shauku kubwa ya kuanza kutumia umeme kwakuwa wamechoshwa na matumizi ya nishati mbadala vikiwemo vibatari,taa za kandiri na mishumaa.

Kijana Hamisi alisema kwa kukosekana kwa umeme kijiji cha kimeendelea kusuasua kimaendeleo kwakuwa shughuli nyingi hivi sasa zinahitaji nishati hiyo ili kuendana na ulimwengu wa sayansi na teknolojia.

Alisema kwa sasa njia pekee inayotumika kuwasaidia wakazi wa kijiji hicho na vingine vya jirani katika kupata mwanga nyakati za usiku na pia kuchaji simu ni umeme wa nishati ya jua aliosema kimsingi hautosjhelezi mahitaji yaliyopo.

“Sola zinatusaidia kuchaji tu simu na kupata mwanga kwa taa chache nyakati za usiku.Umeme huu hauna msaada mkubwa sana kwetu kwakuwa hata sola zenyewe tunazofunga ni ndogo.Tunahitaji umeme wa uhakika kuendesha shughuli zetu ili tuharakishe kupata maendeleo”

“Tunaamini tukipata umeme tutaweza kufanya mambo mengi.Biashaza za vinywaji zitafanyika zaidi kutokana na uwepo wa hali ya joto katika maeneo yetu.Tutaweza pia kufuga kuku kwa njia za kisasa tofauti na sasa” alisisitiza Hamis.


No comments:

Post a Comment