WATU watatu wamefariki dunia mkoani Mbeya katika
matukio tofauti likiwemo la mwanamke mmoja aliyekutwa akiwa ameuawa na watu
wasio fahamika.
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi jana alisema mwanamke huyo aliyefahamika kwa jina la Lucy Yesaya(22) aliuawa kwa
kupigwa na kitu kizito kichwani na usoni.
Alisema mwili wa Lucy ulikutwa ukiwa na majeraha
mnamo Novemba 11 saa 12:30 asubuhi katika kijiji cha Izumbwe Sokoni,kata ya
Songwe wilayani Mbeya.
Alisema jeshi hilo linaendelea na uchunguzi juu ya
tukio hilo sambamba na kuwasaka wauaji ambapo chanzo cha mauaji hayo bado
hakijafahamika.
Katika tukio la pili Mtoto mwenye umri wa mwaka
mmoja na miezi saba Promis Dank mkazi wa Bwawani wilayani Chunya alipefariki dunia
alipokuwa njiani kupelekwa hospitali baada ya kutumbukia kisimani.
Kamanda Msangi alisema mtoto huyo alitumbukia kwenye
kisima chenye maji mnamo novemba 11 saa 12:00 asubuhi katika kitongoji cha
Railway mtaa na kata ya Bwawani.
“Inadaiwa kuwa mtoto huyo baada ya kutumbukia kwenye
kisima ambacho kilikuwa wazi aliokolewa akiwa hai lakini alifariki dunia akiwa
njiani kuelekea hospitali teule ya Mwambani iliyopo Mkwajuni kwaajili ya
matibabu” alisema Kamanda Msangi.
Akizungumzia tukio la tatu,kamanda huyo alisema
mpanda baiskeli wa kiume ambaye hakufahamika jina lake anayekadiriwa kuwa na
umri wa kati ya miaka 25 na 28 alifariki dunia papo hapo baada ya kugongwa na
gari lenye namba za usajiri T 838 AAC
aina ya Toyota Hiace iliyokuwa ikiendeshwa na Deo Mbilinyi.
Alisema ajali hiyo ilitokea novemba 11 saa 10:40
jioni maeneo ya Uyole jijini Mbeya na chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi wa
gari ambapo dereva alikimbia mara baada ya tukio na anatafutwa na polisi.
No comments:
Post a Comment