Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, November 4, 2015

SHITAMBALA AKUBALI YAISHE,AAHIDI KUTEKELEZA AHADI NJE YA BUNGE

ALIYEKUWA mgombea wa ubunge Mbeya mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM) Sambwee Shitambala amempongeza mshindi wa nafasi hiyo kupitia Chadema Joseph Mbilinyi(Sugu) na kubainisha kuwa hana mpango wa kwenda mahakamani kupinga matokeo.

Katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu Shitambala alishika nafasi ya pili akipata kura 46,894 huku Mbilinyi akimshinda kwa kupata jumla ya kura 97,675.

Katika tamko lake alilolitoa kwa vyombo vya habari leo(Nov 4),Shitambala amesema hana mpango wa kwenda mahakamani kupinga matokeo hayo kwakuwa kufanya kutachelewesha mpango wake wa kuwatumikia wananchi nje ya nafasi ya ubunge.

Amesema pamoja na kukosa nafasi hiyo,hatosita kutekeleza ahadi zote alizoziahidi kwa wakazi wa kata zote za jijini hapa lengo likiwa ni kuondoa adha zinazoikabili jamii.


Amezitaja baadhi ya ahadi atakazozitekeleza japo hakuchaguliwa kuwa ni pamoja na ujenzi wa zahanati katika kata za Iyunga, Igawilo, Ilemi na Nsoho, Shule katika kata ya Iziwa, na nyinginezo, usafiri wa daladala pembezoni mwa mji, maji na umeme na pia kutafuta waalimu wazuri kwa ajili ya shule za jijini hapa.

Amesema pia hatosita kumkumbusha rais mteule Dk.John Pombe Magufuli juu ya ahadi alizotoa kwa wakazi wa jiji la Mbeya ikiwemo ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa kilometa 10 kwa kiwango cha lami.


No comments:

Post a Comment