Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, October 29, 2013

Mbeya City waichapa Tanzania Prisons 2-0

MCHEZO wa ligi kuu ya Tanzania bara kati ya Mbeya City na Tanzania Prisons zote za jijini Mbeya umemalizika kwa wenyeji wa mchezo huo Prisons kuambulia kipigo cha goli 2-0. Ndani ya uwanja wa sokoine hadi kipindi cha kwanza kinamalizika hakuna timu iliyokuwa imefanikiwa kulioana lango la mwenzake na kufanya timu hizo kwenda mapumziko zikiwa bila kwa bila huku katika kipindi hicho timu zote zikiwa zimeonyesha uwezo sawa. Mabadiliko waliyoyafanya Mbeya City baada ya kuanza kwa kipindi cha pili ya kumtoa Alex Seth na kumwingiza Peter Mapunda yalionekana kuanza kuleta neema kwa timu hiyo baada ya Dakika ya 62 Mapunda kupachika bao safi akitumia mbwembwe zilizofanywa na mmoja wa walinzi wa Tanzania Prisons Julius Kiwan. Goli hilo lilionekana kuwapa wakati mgumu wajelajela kiasi cha wachezaji kuweza kupoteana uwanjani na ndipo dakika ya 69 Laurian Mpalile wa timu hiyo akajikuta anafanya madhambi eneo la hatari kwa kumvuta Deus Kaseke wa Mbeya City na mwamuzi Israel Nkonga kutoka Dar es salaam kuamuru ipigwe penati. Penati iliyopigwa kiufundi na Deogratius Julius iliiwezesha Mbeya City kujipatia goli la pili na kuiwezesha kuibuka na ushindi wa goli mbili 2-0 mbele ya ndugu zao Tanzania Prison.

No comments:

Post a Comment