Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, October 30, 2013

WATANO WANUSURIKA KATIKA AJALI ZA MALORI

WATU watano wamenusurika kifo katika ajali mbili tofauti zilizotokea mkoani Mbeya jana (oktoba 29) katika maeneo na nyakati tofauti. Ajali ya kwanza ilitokea majira ya saa 5:00 asubuhi katika kijiji cha Isyonje wilayani Mbeya ambapo gari lenye namba T 885 CBS aina ya Scania yenye tela namba T 319 CBU iliyokuwa ikitokea Dar es salaam kuelekea nchini Malawi ikiwa na mifuko 600 ya Mbolea aina ya Urea iliacha njia na kupindika. Lyamba Lya Mfipa ilifika eneo la tukio na kushuhudia wakazi wa maeneo ya jirani wakijibebea mifuko ya Mbolea kwa kubeba kichwani na wengine pikipiki. Baadhi ya wakazi na polisi waliokutwa eneo la tukio na kuomba kutoandikwa majina yao kwakuwa si wasemaji walimtaja dereva kuwa ni George Mwanakulya ambaye hadi wakatio huo yeye na kondakta wake walikuwa wamekimbizwa hospitali ya rufaa Mbeya kwaajili ya matibabu. Ajali ya pili ilitokea majira ya saa 5:40 katika eneo la mlima wa Igawiro ambapo gari yenye namba T 320 BRQ na aina ya Scania na tela namba T 539 BRP ikiwa imebeba mzigo wa viazi mviringo liliacha njia na kupinduka na kusababisha majeraha kwa watu watatu akiwemo dereva lakini wote hawakufahamika.

No comments:

Post a Comment