Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Wednesday, October 30, 2013

MBEYA CITY,TANZANIA PRISONS ZAINGIZA MILIONI 31

MCHEZO wa ligi kuu Tanzania bara uliozikutanisha Mbeya City na Tanzania Prisons zote za mkoani Mbeya uliingiza jumla ya shilingi 31,67400. Akitangaza mapato hayo kwa waandishi wa habari,katibu wa chama cha soka mkoani Mbeya Haroub Suleiman alisema katika mchezo huo uliochezwa jumanne hii ndani ya uwanja wa Sokoine jijini hapa jumla ya watazamani 10,558 waliingia uwanjani kwa kiingilio cha shilingi 3000 kila mmoja. Seleman alisema mgawanyo wa mapato hayo ulifanyika kwa kila timu kuvuna kiasi cha shilingi 6,987,022 kila moja kodi ya ongezeko la thamani ikiwa ni shilingi 4,831,627. Alisema gharama za uwanja ilikuwa shilingi 3,552,723.42,gharama za tiketi shilingi 3,157,550.20,gharama za mechi 2,131,634 na kamati ya ligi shilingi 2,131,634. Mfuko wa maendeleo ya mpira ya Shirikisho la Soka nchini(TFF) ulivuna shilingi 1,065,817 huku chama cha soka mkoa yaani MREFA kikiambulia shilingi 828,968.79. Katibu huyo aliwashukuru mashabiki waliojitokeza uwanjani hapo kushuhudia mchezo huo ambao ulimalizika kwa wenyeji wa mchezo Tanzani Prison kuambulia kichapo cha goli 2-0 kutoka kwa wadogo zao wabishi wa ligi Mbeya City.

No comments:

Post a Comment