Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, October 10, 2013

WATATU WAAMSHA MAISHA YAO NA COCACOLA KWA KUJISHINDIA PIKIPIKI

Meneja mauzo na masoko wa kiwanda cha Cocacola kwanza cha mkoani Mbeya Vekaria Jayanti akimkabidhi mfano wa hundi ya kitita cha shilingi milioni moja Frank John mkazi wa Sumbawanga mkoani Rukwa baada ya kubahatika katika promosheni ya Amsha maisha yako na Cocacola. MKAZI wa Chunya mkoani Mbeya Alex Mtweve na mkazi wa Soweto jijini hapa Jackson Mwamsonga ni miongoni mwa watu watatu waliojishindia pikipiki aina ya Yamaha zenye thamani ya shilingi milioni 2.5 kila moja katika promosheni ya Amsha Maisha yako na Cocacola. Mshindi wa tatu wa promosheni hiyo aliyejishindia pikipiki pia katika promosheni hiyo inayoendeshwa na kampuni ya vinywaji baridi ya Coca Cola ni mkazi wa Songea mkoani Ruvuma Alex Manga. Meneja mauzo na masoko wa kiwanda cha Coca Cola Kwanza cha mkoani hapa Vekaria Jayanti alikabidhi pikipiki hizo jana kwa washindi katika hafla fupi iliyofanyika kwenye kituo kidogo cha mabasi cha Kabwe jijini hapa. Jayanti pia alikabidhi fedha taslimu kwa washindi wa viwango vya milioni moja moja kwa watu wawili na shilingi laki tano kila mmoja kwa washindi watatu. Waliokabidhiwa shilingi milioni moja kila mmoja ni mkazi wa Sumbawanga mkoani Rukwa Frank John na mkazi wa Iringa Rahim Mwanuka. Waliojishindia shilingi laki tano kila mmoja na mkazi wa Mwanjelwa jijini hapa Daud Mwangomba,Edgar Sanga mkazi wa Kamsamba wilayani Momba na John Ngawanya mkazi wa Iringa. Akikabidhi zawadi kwa washindi,Jayanti aliwataka kuzitumia kuinua kipato cha familia zao ili malengo ya kampuni hiyo ya kuboresha maisha ya wateja wao yaweze kutimia. “Lengo la kampuni ni kuona maisha ya wateja wanaonunua vinywaji vyetu yanakuwa bora zaidi.Ndiyo sababu plomosheni yenyewe ikaitwa amsha maisha.Sasa ni vema mkatumia zawadi hizi kuboresha maisha ya familia zenu ili kampuni ijione imetimiza wajibu wa kuamsha maisha ya wateja wake” alisema Jayanti. Mmoja wa washindi wa pikipiki Alex Mtweve mkazi wa Chunya aliishukuru kampuni hiyo akisema imemwezesha kuachana na pikipiki ya mtu aliyokuwa akiendesha awali akisafirisha abiria maarufu kama bodaboda na sasa taendesha yak wake mwenyewe.

No comments:

Post a Comment