Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, October 27, 2013

WATANO WAUAWA KINYAMA CHUNYA

WATU watano wameuawa kikatili katika matukio mawili tofauti yaliyotokea wilayani Chunya mkoani Mbeya moja likisababishwa na imani za kishirikina na la pili ikiwa ni wivu wa mapenzi. Tukio la kwanza lilitokea Oktoba 25 mwaka huu majira ya saa 2:00 usiku katika kijiji cha Mpona kata ya Totowe tarafa ya Songwe ambapo kikongwe na mkazi wa kijiji hicho Jampany Mhamali(78) akiwa njiani kurudi nyumbani akitokea kwenye kilabu cha pombe za kienyeji alivamiwa na watu wawili wasiofahamika na kukatwakatwa mapanga kichwani na mkono wake wa kulia hadi kufa. Baada ya wakazi wa kijiji hicho kupata taarifa za mauaji hayo walijikusanya wakiwa na silaha za jadi ikiwemo mawe na kuanzisha msako mkali kwa kufuata nyayo za viatu vya watu waliotuhumiwa kuhusika na baadaye wakafanikiwa kuwakamata watu hao ambao hawakufahamika majina na kuanza kuwashushia kipigo na kuwaua wote wawili. Hata hivyo wakati wakiendelea kupigwa watuhumiwa hao walikiri kuhusika na mauaji ya kikongwe Mhamali na kueleza kuwa wao walitumwa na Maneno Adamson maarufu kwa jina la Lyambo ambaye alikuwa akimtuhumu kikongwe huyo kuwa ni mchawi. Wanachi hao baada ya kuwaua watuhumiwa wawili walikwenda moja kwa moja nyumbani kwa mtuhumiwa wa tatu akliyetajwa kuwaagiza watu hao lakini kwa bahati mbaya hawakufanikiwa kumkuta kwani alikuwa amekwisha toroka. Tukio la pili ni la kuuawa kwa kuteketezwa kwa moto kwa Adelina Philimon(45) mkazi wa kijiji cha Magamba wilayani hapa na Wasiwasi Mwashiombo(28) mkazi wa kijiji cha Ipoloto Wilayani Mbozi. Wapenzi hao ambao kiumri ni sawa na mama na mtoto wake waliteketea kwa moto baada ya nyumba waliyokuwa wamelala kuchomwa moto na mtu aliyetajwa kwa jina la Zacharia Mwingila(39) mkazi wa Tunduma wilayani Momba. Chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa kimapenzi ambapo mtuhumiwa ambaye kwa sasa anashikiliwa na polisi alifikia hatua ya kuchoma moto nyumba baada ya kumkuta mpenzi wake akiwa amelala na mwanaume mwingine amjira ya saa tano za usiku wa oktoba 25 mwaka huu katika kijiji cha Magamba wilayani Chunya. Kaimu kamanda wa polisi mkoani Mbeya Robert Mayala alithibitisha kutokea kwa matukio hayo yote mawili na kuisihi jamii kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mikononi na pia kuishi kwa kuwatumhumu wakazi wenzao wakiwahusisha na imani za kishirikina.

No comments:

Post a Comment