Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Thursday, October 10, 2013

WACHUMBIA NDIZI MASHAMBANI KUKIONA CHA MOTO

WACHUMBIAJI wa ndizi wilayani Rungwe wamepewa muda wa wiki mbili kuainisha madai yao kwa wakulima na kuyafikisha katika ofisi za watendaji wa vijiji kwakuwa sasa ni marufuku kufanyika kwa biashara hiyo. Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispini Meela amewataka wafanyabiashara waliochumbia ndizi kuhakikisha wanatekeleza agizo hilo kwakuwa kuanzia Novemba Mosi mwaka huu biashara hiyo haitoruhusiwa tena wilayani hapa. Meela alitoa agizo hilo jana katika kijiji cha Lugombo kata ya Lufingo wilayani hapa alipozindua muungano wa vikundi vidogo vya wakulima wa ndizi na kahawa bora(WANDIKARU). Alisema kwa muda mrefu wakulima wilayani hapa wameendelea kuwa masikini kutokana na kunyonywa kwa kiasi kikubwa na wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiwauzia mikungu ya ndizi change ikiwa bado mashambani hivyo wao wakulima kubaki wakiitunza kungoja ikomae wenye nayo waje kuivuna. Alisema haiwezekani kumsaidia mkulima wa ndizi wilayani hapa pasipo kufanya mamuzi magumu kama hayop hivyo sasa wafanyabiashara wachumbia ndizi imefika wakati wao kutafuta utaratibu mwingine na si waliouzoea. Alisema baada ya muda uliopangwa kupita itakuwa imekula kwa wafanyabiashara kwakuwa hakuna polisi,mahakama,wala mtendaji wa kijiji atakayepokea kesi ya kuchumbia nzidi na atakayepeleka kesi ya namna hiyo huyo atakamatwa. Alisema kuanzia sasa wakulima watapaswa kupeleka ndizi zao kwenye vituo vitakavyotengwa na vijiji na huko ndiko watakutana na wafanyabiashara watakaonunua kutoka kwao. Mkakati mwingine ni kufunguliwa kwa magulio maalumu ya kuuzia ndizi ambapo kwa halmashauri ya Rungwe limetengwa eneo la Karasha na halmashauri ya Busokelo eneo litakuwa Lwangwa. Awali mwenyekiti wa Wandikaru Lusekelo Mwakibete alisema muungano huo unatokana na vikundi 16 kutoka kata tofauti za wilayani hapa huku akibainisha ukosefu wa masoko maalumu vijijini kuwa moja ya changamoto inayochangia wafanyabiashara kuwarubuni wakulima kuwauzia ndizi mashambani.

No comments:

Post a Comment