Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Monday, October 14, 2013

MOTO WATEKETEZA MKE NA MUME

MUME na mke wamefariki dunia kwa kuungua moto baada ya nyumba yao kuteketea kwa moto. Wanandoa hao wamefahamika kwa majina ya Fadhir Said(45) na Lucy Said ambaye umri haufahamiki wote wakazi wa Ilemi jijini Mbeya. Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwani Athuman tukio hilo lilitokea majira ya saa sita usiku wa kuamkia leo(Oktoba 14) nyumbani kwao huko Ilemi. Kamanda Athuman alisema chanzo cha moto ulioteketeza nyumba hiyo yenye vyumba sita hakijajulikana na kuwa watoto wanne waliokolewa kabla ya kupata madhara. “Wananchi na polisi waliofika eneo la tukio walifanikiwa kuzima moto huo lakini ukiwa tayari umesababisha madhara ya vifo hivyo pamoja na kuteketeza mali mbalimbali ambazo thamani yake bado haijajulikana” alisema. Wakati huo huo jeshi hilo linamshikilia fundi magari mkazi wa kijiji cha Ilembo wilayani Mbozi Erick Kyando(32) baada ya kukamatwa akuiwa na noti bandia zenye thamani ya shilingi 100,000. Kamanda huyo alisema mtuhumiwa alikamatwa oktoba 13,saa 12 jioni katika mji mdogo wa Mlowo wilayani hapo akiwa na noti kumi bandia za shilingi elfu kumi kila moja zikiwa mpya. Mshitakiwa huyo alikamatwa wakati alipofika kwa wakala wa M-Pesa aitwaye Lydia Mwakipesile akitaka kuziweka katika akaunti yake.

No comments:

Post a Comment