Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, July 14, 2015

MWANAHABARI ATANGAZA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA VIJIJINI













MWANAHABARI Gordon Kalulunga ametangaza nia ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) wilayani hapa kumpa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho akigombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Mbeya vijijini kwenye uchaguzi mkuu ujao.

Kalulunga alitangaza nia hiyo alipozungumza na waandishi wa habari kwenye viwanja vya Mahubiri vilivyopo katika mji mdogo wa Mbalizi wilayani hapa,mkutano uliohudhuriwa pia na wakazi mbalimbali kutoka ndani na nje ya mji huo.

Akizungumzia nia hiyo,Kalulunga alisema anawania nafasi ya ubunge wa jimbo hilo kwa lengo la kuwatumikia wananchi na kamwe si kwaajili ya kupata kinga kwa shughuli zozote zenye maslahi yake binafsi.

Alisema kwa muda mrefu kumekuwa na tabia jimboni hapa ya viongozi kujitokeza kugombea nyadhifa mbalimbali wakilenga kupata nafasi ya kuutumia uongozi kama kinga kwa biashara wanazofanya.

“Sigombei ili nilinde maslahi ya shughuli ninazofanya,wala kulinda kabila lolote.Nagombea ili niwatumikie wakazi wa jimbo la Mbeya vijijini.Tunapowachagua watu wanaotaka kulinda maslahi yao tutabaki kulalamikia serikali kuwa haituletei maendeleo lakini ukweli ni kuwa tutakuwa tumewasaidia watu wachache kutimiza malengo yao”

“Wilaya yetu ni wilaya inayopakana na wilaya karibu zote za mkoa wa Mbeya isipokuwa wilaya za Kyela na Momba lakini ni wilaya isiyokuwa na hata chuo kimoja kinachotoa walau taaluma yoyote hata katika ngazi ya cheti.Ni kwa sababu hatujapata viongozi wenye uchungu na maisha yetu” alisisitiza Kalulunga.

Mwanahabari huyo alisema iwapo atapewa nafasi na CCM na kuweza kuukwaa ubunge wa jimbo hilo,sambamba na kutekeeza ilani ya chama hicho,pia kipaumbele chake kikuu ni afya ya jamii kwanza.

Alisema kwake Afya anaipa kipaumbele kwakuwa mtu yeyeto aliye na afya njema ataweza kushirikia katika mikakati mbalimbali ya kujiletea maendeleo yeye binafsi,jamii inayomzunguka na taifa kwa ujumla.
Alisema endapo Chama chake kitampitisha na hatimaye kushinda Ubunge katika Jimbo hilo atahakikisha wananchi wote wanajiunga na mfuko wa bima ya afya kwa ajili ya matibabu kwa kila kaya kuchangia ili kupunguza adha na gharama kubwa za matibabu.

Aliongeza kuwa akifaniiwa kuukwaa Ubunge pia atasimamia kuhakikisha Jimbo hilo linapata Chuo cha aina yoyote kikiwemo Chuo cha ufundi kwa ajili ya vijana kupata elimu jambo lilatalopunguza wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana.

No comments:

Post a Comment