Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, July 14, 2015

WANACCM IWAMBI WAJITOLEA KUKARABATI JENGO LA DARASA









 JAMII mkoani Mbeya imehimizwa  kujitolea kwenye uttafutaji wa suluhu za changamoto zilizopo kwenye maeneo yao badala ya kubaki wakisubiri serikali kutekeleza kila jambo.

Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) kata ya Iwambi jijini Mbeya walitoa hamasa hiyo kwenye shughuli ya ukarabati wa jengo la darasa la Kidato cha kwanza B lililopo katika shule ya sekondari ya Iwambi ambapo wanachama wa chama hicho wameamua kujitolea kulikarabati.

Mwenyekiti wa CCM kata ya Iwambi Cyprian Gamba amesema wamehamasika kukarabati jengo hilo ikiwa ni ahadai waliyoitoa kwenye ziara ya Waziri mkuu Mizengo Pinda alipotembelea shule hiyo kwaajili ya kuzindua maabara.

Akizungumza na Lyamba Lya Mfipa Mapema leo shuleni hapo,Gamba amesema wanachama wa CCM kata ya Iwambi wameguswa na kilio cha wanafunzi na walimu shuleni hapo na kuona haja ya kukarabati moja ya majengo yaliyo na hali mbaya.

Amesema ni wakati kwa jamii kubadili mrtazamo kwa kushiriki kutatua changamoto ndogo ndogo kwenye maeneo yao badala ya kuiachia serikali kutekeleza kila jambo.

Kwa upande wake katibu wa CCM kata ya Iwambi Geoge Nyirenda amesema wameamua kuchanga michango na kwa kuanza wamefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi laki sita na lengo ni kuboresha chumba cha darsa hilo kuanzia sakafu hadi madirisha.

Nyirenda ameitaka jamii kutouhusisha mchango huo na harakati za kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu ujao huku akisema huo ni mchango wa wanaccm katika maendeleo ya kata na ndiyo sababu haujatolewa na mtu mmoja.

No comments:

Post a Comment