Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Sunday, August 11, 2013

AUA MKEWE KWA KUMNYONGA SHINGO.KISA WIVU WA MAPENZI

POLISI mkoani Meya inamshikila mkazi wa kijiji cha Mapogoro kata ya Miombweni wilayani Mbarali kwa tuhuma za mauaji ya mkewe kutokana na wivu wa mapenzi. Anayeshikiliwa na jeshi hilo amefahamika kwa jina la Nkuva Malale(39) ambapo inadaiwa kuwa alimuua mkewe kwa kumpiga fimbo maeneo mbalimbali ya mwili wake ikiwemo maeneo ya kichwani kabla ya kumnyonga shingo. Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Diwan Athuman jana aliwaambia wandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea agosti 10 mwaka huu majira ya saa 10:30 kijijini Mapogoro. Kamanda Athuman alimtaja aliyeuawa katika tukio hilo la kinyama kuwa ni Mbuke Ochegeri(34) aliyekuwa mkulima na mkazi wa kijiji hicho. Alisema kabla ya kumshushia kipigo na kisha kumuua mtuhumiwa wa mauaji alikuwa akimtuhumu mkewe kuwa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine. Aidha alisema uchughuzi zaidi juu ya mauaji hayo unaendelea na kubainisha kuwa wakati wowote mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.

No comments:

Post a Comment