Karibu katika blogu hii,kuwa mmoja wa wale wanaochangia na kujivunia mafanikio yake. Tunakualika kwa mikono miwili wasiliana nasi kwa simu 0756409597 au nyambojoachim@gmail.com

Tuesday, August 6, 2013

SUMAYE AZUNGUMZIA KATIBA MPYA

WAZIRI mkuu mstaafu Frederick Sumaye amesema tume ya katiba haipaswi kuwa na msimamo wake kuhusu maoni yaliyotolewa na wananchi kwakuwa imekwisha yaweka kwenye rasimu. Badala yake ameitaka tume hiyo kuyaachia mabalaza ya katiba kujadili rasimu hiyo kwakuwa kuendelea kuweka msimamo inamaanisha nayo ina msimamo wake inaotaka upitishwe na mabalaza hayo. Sumaye aliyasema hayo jana alipokuwa akifunga mkutano wa siku mbili wa balaza la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu(Tahliso) uliofanyika katika chuo kikuu cha Mzumbe tawi la Mbeya likiwakutanisha na viongozi mbalimbali wa serikali ya wanafunzi wa vyuo hivyo. Alisema ili mradi kazi ya tume ilikuwa kuratibu maoni ya wananchi,basi haipaswi pia kulaumiwa kwa maoni yaliyotolewa isipokuwa kama imetoa rasimu isiyowakilisha maoni na wananchi walivyoyatoa. “Wakati wakutoa maoni yao bila shaka wapo watanzania waliotaka serikali moja,wapo waliotaka serikali mbili,waliotaka serikali tatu,waliotaka serikali nne,labda wapo waliotaka serikali ya mkataba na inawezekana labda wapo waliotaka tuachane na muungano” “Kila mmoja aliyetoa maoni yake alikuwa na haki ya kufanya hivyo kikatiba na sababu ya kutoa maoni yake hayo kama alivyotaka.Hivyo si sahihi mtu au kundi la watu kukejeli au hata kutukana mtu au kundi linguine lililotoa maoni yanayotofautiana na yake au kundi lake” alisema Aliwataka watanzania kujifunza ustahimilivu na kuheshimu maoni aumawazo ya watu wengine na kama hawakubaliani nayo wayapinge kwa nguvu ya hoja na si hoja ya nguvu. Waziri mkuu huyo mstaafu alisema katika kufuatilia mchakato mzima wa katiba mpya nchini amebaini mambo makubwa mawili aliyosema moja ni baadhi ya watanzania kuamini matatizo yaliyopo ya hali ngumu ya maisha na maendeleo duni ya jamii inatokana na katiba iliyopo hivi sasa wanayodhani kuwa ni mbaya. Alisema jambo la pili ni uwepo wa watu wenye fikra kuwa katiba mpya utakuwa muarobaini wa matatizo yote mitazamo aliyosema yote si sahihi na inaweza kupotosha taifa isipoelezwa vizuri. Alisema kwa maoni yake hata katiba iliyopo ni nzuri na ndiyo maana imewezesha kufikia umri wa karibu miaka 50 katika muungano watanzania wakiwa salamaa na kuna mshikamano mzuri nchini. Aliongeza kuwa kwa vyovyote katika miaka 50 kuna mabadiliko mengi yametokea katika jamii hivyo katiba hiyo ingebidi tu kuhitaji marekebisho kama ambavyo hata hiyo mpya itahitaji marekebisho baadaye kutokana na mahitaji ya jamii. Aidha Sumaye pia alisisitiza umuhimu wa watanzania kukumbuka kuilinda katiba yao huku akisema mtu muhimu na wa kwanza kuilinda katika ya nchi ni rais.

No comments:

Post a Comment